Tamasha la Urembo wa Asili Tanzania kufanyika kesho Jumamosi na keshokutwa jumapili Viwanja vya life park mwenge ilipo Maisha club ,zamani Sinema mwenge. 

Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mh Naibu waziri wa Habari , Utamaduni, sanaa na michezo Bi Juliana shonza .

Tamasha hili litakua na faida kwa kila atakefika bila gharama yoyote itatolewa huduma ya vipimo vya kansa ya Titi pamoja elimu ya kansa na magonjwa ya ngozi bure kutoka kwa wataalam Ocean Road

Vile vile kutakua na mafunzo ya ujasiriamali utengezaji wa sabuni za maji za kuogea ( shampoo ) bure kutoka kwa mjasiriamali na mwalimu Bi. Ester Mgonja bure siku ya jumapili .

Burudani itaongozwa na Malkia wa Taarabu Khadija Kopa pamoja na Aneth kushaba, mtangazaji na mjasiriamali Dina Marious na Sakina Lyoka watakuwepo , wasanii mwasiti, Grace matata, mchekeshaji jaymond watakuwepo na Rose Ndauka atakuwepo, kutakua Fashion show na burudani ya muziki ya kutosha. 

Sherehe za Urembo wa asili zitaambatana na kutoa zawadi kwa wanawake 300 watakaofika wa kwanza viwanja ni hapo kujipatia zawadi ya pakti moja ya Pedi ya kutoka Belle Bure.

Njoo ukutane na Wajasiriamali wa bidhaa za Urembo wa ngozi na nywele na bidhaa zingine kuanzia asubuhi saa 2 hadi saa 12 jioni. Vyakula na vinywaji vitapatikana pia. 

Urembo wa Asili sio ushamba .
@tanzanianaturalbeautyday
@missmandoza

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...