Na Zainab Nyamka, Michuzi Tv

KIKOSI cha Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu Tanzania (Taifa Stars) kimeshindwa kufanya vyema kwenye uwanja wake wa nyumbani baada ya kulazimishwa suluhu ya kutokufungana na timu ya Taifa ya Kenya 'Harambee Stars'.

Mchezo huo wa kufuzu michuano ya wachezaji wa ndani CHAN umefanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa kwa kuzikutanisha timu hizo.

Kaimu Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Ettiene Ndayiragije amesema mchezo ulikuwa ni mzuri kuna mapungufu ameyaona ila atakaa na wachezaji kuweza kuyafanyia kazi.

"Tutaenda kufanyia kazi mapungufu yaliyojitojeza na kwenda kusaka ushindi katika michezo wa marudiano nchini Kenya na kushindwa kupata matokeo leo haimaanishi tutashindwa kufuzu," amesema Ndayiragije.

Katika mchezo wa leo, Taifa Stars imeshindwa kupata matokeo katika mchezo wa leo na Kocha amesema anaamini lengo la vijana wake ni kupambana kwenye mchezo wa marudiano.

Sasa Stars italazimika kushinda ugenini kwenye mchezo wa marudiano utakaochezwa nchini Kenya Agosti 4.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...