Pichani kulia ni Naibu Katibu Mkuu (EAC),Christopher Bazivamo akizungumza kwenye Warsha ya siku moja mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) hivi karibuni kuhusu mradi wa 50 Milioni African Women Speak Networking,unaotarajiwa kuratibiwa nchini Tanzania ili kuwaunganisha wanawake Wajasiriamali katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki,Kushoto ni
Mkurugenzi wa Idara ya Jamii (EAC),Mary Makoffu.Picha na Michuzi JR.
Warsha hiyo ya Wanahabari ikendelea
 Naibu Katibu Mkuu (EAC),Christopher Bazivamo akifafanua zaidi kwenye Warsha ya siku moja mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) hivi karibuni kuhusu mradi wa 50 Milioni African Women Speak Networking,unaotarajiwa kuratibiwa nchini Tanzania ili kuwaunganisha wanawake ,pia katika nchi za Ecowas na Commesa  na lengo lake kubwa ni kuwawezesha wanawake kiuchumi na hususani wanawake wajasiriamali,Pichani kulia ni  Mkurugenzi wa Fedha (EAC) Juvenari Ndimurirwo na  kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Jamii (EAC),Mary Makoffu
Mkurugenzi wa Idara ya Jamii (EAC),Mary Makoffu(katikati) akizungumza mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani),kwenye Warsha hiyo ya siku moja iliofanyika jijini Dar,kushoto ni Ofisa Maendeleo Mwandamizi wa Wizara hiyo kutoka Idara ya Jinsia Mapunda John
Mratibu wa Mradi wa 50 Milioni African Women Speak Networking,Bw. Wilson Muyenzi akiwasilisha mada kwa waandishi wa habari katika semina hiyo.
Mkurugenzi wa Fedha (EAC) Juvenari Ndimurirwo akifafanua namna ya umuhimu wa kupanga na matumizi ya fedha katika mambo mbalimbali ikiwemo mradi wa Mradi wa 50 Milioni African Women Speak Networking,hasa kwa watakaosiriki kwa namna moja ama nyingine.

Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii.

WIZARA ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto imeeleza faida za upatikanaji wa taarifa muhimu zikiwemo za fedha kwa Wanawake wajasriamali kwa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki na nchi nyingine Barani Afrika.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Ofisa Maendeleo Mwandamizi wa Wizara hiyo kutoka Idara ya Jinsia Mapunda John amesema wajasiriamali hao wanaunganishwa kupitia mradi wa 50 Milioni African Women Speak Networking.

Amesema ni mradi ambao unatekelezwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki,pia katika nchi za Ecowas na Commesa  na lengo lake kubwa ni kuwawezesha wanawake kiuchumi na hususani wanawake wajasiriamali.

"Kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki mradi unatekelezwa kwenye nchi sita. Na sio jumuiya ya Afrika Mashariki tu bali hata katika nchi nyingine nje. Kuhusu kuwawezesha wanawake kiuchumi ni katika suala zima la kuwapatia taarifa muhimu ikiwa pamoja na taarifa za fedha na taarifa ambazo sio za fedha.

"Sasa kwa maana ya taarifa za fedha tunamaanisha taarifa kwa mfano za wapi mikopo inapatikana ,wapi grants zinapatikana lakini ili waweze kutumia kama mitaji kuendesha biashara zao lakini tunavyosema taarifa ambazo sio za fedha kuna taarifa mbalimbali ambazo ni muhimu kwa wajasiriamali kuzipata," amesema John.

Pia amesema taarifa zinazohusu masoko na mambo mengine ya kutambua thaman na wapi kwenye uhitaji na hata usalama wa biashara kwani kuna baadhi ya nchi nyakati za uchaguzi hahuko salama ,hivyo lazima wajasiriamali hao wawe na taarifa.

Amesisitiza kwamba lengo kubwa la mradi huo ni kuhakikisha ni namna gani taarifa hizo zitawafikia wanawake wajasiriamali na ndio maana matarajio ni kuandaliwa kwa Website ambayo ndani yake kutakuwa kunawekwa taarifa zote muhimu.

"Na kwamba si tu bali wanafikiria kwa kuwa na eneo moja la wajasiriamali kukutana watakuwa na mijadala mbalimbali kati ya wafanyabiashara wakubwa na wakati ikiwa pamoja na kubadilishana uzoefu," amesema John.

Amefafanua kuwa wameona kuwa wanaweza kutengeneza Website nzuri na kuwekwa taarifa zote lakini kama wanawake wajasiriamali hawajui haitakuwa na maana yoyote.

Hivyo amesemani fursa muhimu kwao kukutana na vyombo vya habari kwani kwa kutumia njia zao za kufikisha taarifa watawafikishia wanawake wajasiriamali taarifa za nchiradi huo  na wanafanya hivyo kwa kuamini kuna takribani ya wanawake milioni 500 na malengo ni kuwafikia wanawake asilimia 10 ambayo ukiiigiwa unapata wajasiriamali milioni 50 kwa jumuiya tatu ambazo kuna nchi 38.

"Wanawake wapo wengi,wapo ambao wamefanikiwa na wapo ambao hawajafanikiwa.Kwa kutumia Poto hii au Website tunaamini itakuww chachu ya maendeleo yao na nchi husika kwa ujumla," amesema John.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...