Baadhi ya Bidhaa zilizopigwa marufuku na TBS kama zinavyoonekana katika picha
Bidhaa hizo zilizopigwa marufuku na TBS zikiteketezwa


Na Vero Ignatus,Arusha.

Shirika la viwango nchini Tanzania (TBS) limeendesha zoezi la kuteketeza bidhaa zilizopigwa ma ndani za mitumba pamoja na vilainishi vya magari visivyo na ubora vilivyokamatwa katika masoko mbalimbali mkoani Arusha.

Fundi Sanifu wa Ukaguzi kutoka TBS Godifrey Nguma amesema uteketezaji wa bidhaa hizo zinazofikia jumla ya tani 2 zilizoteketezwa katika dampo kuu LA mkoa wa Arusha lililoko kata ya Muriet jijini Arusha ,amesema kuwa nguo za ndani za mitumba zina madhara makubwa ikiwemo kusababisha magonjwa sugu kwa watumiaji hivyo zoezi LA uteketezaji linalenga kulinda afya za wananchi.

Stanford Matei ni Ofisa Mdhibiti kutoka shirika hilo mesema kuwa zoezi hilo limefanyika kwa mujibu wa sheria ili kuhakikisha kuwa bidhaa hizo zinaondolewa masokoni pia kufanya juhudi za kudhibiti uingizwaji wa bidhaa zisizokidhi viwango zinazoingizwa kwa njia za panya .

Mkazi wa Arusha Amir Hemed amesema kuwa operesheheni hiyo ya kuteketeza bidhaa zilizopigwa marufuku katika masoko inapaswa kuwa endelevu ili kuhakikisha kuwa bidhaa hizo zinaondolewa sokoni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...