Wananchi waliofika katika maonesho ya 43 ya Kimataifa ya Biashara Sabasaba 2019 wakiuliza maswali kwa timu ya wataalamu kutoka Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) walipotembelea banda hilo lililopo jengo la Saba Saba Hall kujionea shughuli zinazofanywa na mamlaka hiyo. Wananchi waliojitokeza katika banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA)  wakipewa elimu juu ya masuala ya usalama na usafiri wa anga. Mkufunzi wa Chuo cha Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC) Thamarat Abeid (kushoto) akitoa elimu kwa wanafunzi waliotembelea banda la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kujifunza masuala mbali mbali ya Usalama wa anga. Mhandisi Edina Mbwana wa TCAA akimuelezea mwananchi aliyetembelea banda hilo kujionea namna mitambo ya mawasiliano pamoja na uangalizi wa ndege inavyofanya kazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...