Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC), inatarajia kushiriki kwenye maadhimisho ya sherehe za kitaifa za Nane Nane kanda ya ziwa mashariki yatakayofanyika katika viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu kuanzia tarehe 28 Julai hadi 10 mwezi Agosti, 2019. 

Katika maadhimisho hayo, TAEC itaweza kuonesha shughuli mbali mbali zinazofanyika katika Tume ikiwemo utoaji wa elimu kwa wananchi na wadau mbali mbali juu ya udhibiti na matumizi salama ya mionzi hapa nchini. 

Elimu kwa wananchi kuhusu matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia kwenye sekta za afya, kilimo, viwanda, mifugo, maji, lishe pamoja na ujenzi inatolewa. 

Wananchi wote wanakaribishwa ili kuweza kujipatia elimu bure kwa njia za maelezo, video fupi, vipeperushi na majarida ili kujiongezea uelewa juu ya majukumu yanayotekelezwa kisheria na TAEC katika Nyanja za udhibiti wa mionzi na uhamasishaji wa matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia. 

Imetolewa na , 

Peter Ngamilo 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano 

Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...