Na Charles James

Umoja wa vijana wa Chama cha mapinduzi [UVCCM] Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma umesema kuwa chama hicho kitashinda kwa kishindo kwa asilimia mia moja kwenye mitaa yote ya wilaya hiyo katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa .

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Bahi, Kadoke Hassan wakati akizungumza na Waandishi wa Habari Wilayani humo.

Kadoke amebainisha misingi madhubuti itakayokipaisha chama hicho ni kutokana na Uongozi mzuri na Maridadi wa Rais Dk John Pombe Magufuli ikiwa ni pamoja na ununuzi wa ndege, mradi wa bomba la kusafirishia Mafuta ghafi kutoka Hoima Uganda hadi Tanga Tanzania pamoja na Mradi wa reli ya kisasa.

Mwenyekiti huyo wa UVCCM amehamasisha vijana wote kushikamana na kujitokeza katika ushiriki wa serikali za mitaa na wasisite kuyatangaza Mazuri yanayofanywa na Rais Magufuli.

Aidha ,UVCCM wilaya ya Bahi umechukua fursa ya kumpongeza Mathias Lyamunda aliyekuwa Mgombea wa Ubunge mwaka 2015 kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kwa uamuzi wake wa kujiuzulu nafasi zake ndani ya Chama hicho na kuhamia CCM ili kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais Magufuli na Serikali ya CCM katika kuwaletea maendeleo Watanzania.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Bahi, Kadoke Hassaan akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akizungumzia uchaguzi wa Serikali za Mitaa na namna walivyojipanga kuhakikisha wanashinda mitaa yote.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...