Na Leandra Gabriel,  Michuzi TV 
KATIKA kuhakikisha ajali za barabarani hasa zile zinazosababishwa na pikipiki zinapungua Mamlaka ya elimu na mafunzo ya ufundi stadi (VETA) wamebuni pikipiki salama ambayo itahakikisha usalama wa dereva na abiria unazingatia. 

Akizungumza na Michuzi TV mwalimu wa masuala ya umeme kutoka VETA Kipawa Aneth Mganga amesema kuwa ubunifu huo wa pikipiki salama umewalenga madereva na abiria na hiyo ni katika kuhakikisha usalama wao pamoja na abiria unazingatia. 

Aneth amesema kuwa pikipiki hiyo salama imebuniwa kwa kuhakikisha dereva akitumia pombe, akienda mwendo wa haraka, kutovaa kofia ngumu,   kwenda mwendo mkali pamoja na kubeba abiria zaidi ya mmoja pikipiki hiyo haitaruhusu kabisa,  aidha itagoma kwenda au kumpeleka kwenye mwendo wa wastani kama atakuwa kwenye mwendo wa kasi. 

"Pikipiki hii ina mfumo maalumu dereva akinywa pombe,  asipovaa kofia ngumu na akibeba abiria zaidi ya mmoja haiwezi kuwaka na akienda mwendo wa kasi pikipiki hiyo itampeleka katika mwendo wa kawaida" ameeleza. 

Pia amesema kuwa kutokana na mchango mkubwa wa usafiri huo ambao umetoa ajira kwa vijana na kwa kuangalia changamoto zinazoukabili ikiwemo ajali za barabarani wao Kama wataalamu wakaona ni vyema kuangalia namna ya kutatua changamoto hiyo. 

Na amesema kuwa pikipiki hiyo ina mfumo wa usalama ambao utamsaidia dereva kutoa taarifa katika kituo anachofanyia kazi akiona mashaka juu usalama wake juu ya abiria aliyembeba. 

Pikipiki iyo salama imekuwa kivutio kikubwa katika maonesho ya 43 ya biashara maarufu Kama sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. 
Mkufunzi wa masuala ya umeme kutoka VETA Kipawa Aneth Mganga akionesha pikipiki salama ambayo wameibuni ili kupunguza ajali za barabarani, leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...