Na Woinde Shizza Michuzi Tv,Arusha 

Wazee wa halmashauri ya wilaya ya Arumeru wameiomba serikali kuwasaidia kuwapatia Vitambulisho vya wazee ,vitakavyo wawezesha kupatiwa huduma za afya bure popote pale wanapopata matatizo ya kiafya

Aidha pia wameiomba serikali kiwasaidia kupata huduma za kunusuru kaya maskini na zisizo jiweza (Tasaf )kwani katika vijiji vyao hawajapatiwa na kuna wanavijiji wengi ambao ni maskini na wasiojiweza.

Waliyasema hayo  wakati wakizungumza katika mkutano ulioandaliwa na mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa mkutano wa halimashauri ya wilaya Arusha mkutano uliowashirikisha wazee wa kimila ,viongozi wa dini, pamja na viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa 

Wazee wamesema kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakikumbana na changamoto mbalimbali zikiwemo za ubovu wa miundombinu ya barabara gharama kubwa ya maisha, ukosefu wa mitaji ,huku wakiwataka mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kuwasogezea huduma ya kupata Vitambulisho hivyo karibu kwani sehemu ambayo wameipanga ni mbali na inawapa changamoto kubwa wazee hao kufika.

"Nida walikuja kutoa elimu wakataka tujiandikishe ,na tumejiandikisha sasa wanatuambia tutembee adi halimashauri tukachukue sisi ni wazee tutaendaje uko tutavukaje barabara kwenda huko hivyo tunaiomba serikali itusaidie kuwaambia Nida watusogezee huduma hii kama walivyokuja kutupa elimu katika ofisi za kata watuletee nahivyo Vitambulisho katika kata zetu" alisema mmoja wa wazee hao aliejitambulisha kwa jina la Maxtone Mollel 

Aisha pia wazee hao walitumia mda huo kuiomba serikali kugawanya wilaya ya Arumeru ili waweze kupata huduma kiurahisi karibu na maeneo hao kwani wazee wengine pamoja na wananchi wanalazimika kufata huduma katika makao makuu ya wilaya kwa umbali mrefu ,ambapo walifafanua kubwa walikuwa wakitumia mda mrefu kufata huduma katika makao makuu ya halmashauri ya wilaya hiyo.

"Tunampongeza sana rais magufuli kwa kazi anayofanya kwani kazi a anayofanya ni nzuri na hawa ndio viongozi tuliokuwa tunawataka maana katika uongozi wake tu ameshatuletea mandege ambayo tulikuwa hatuna sasa ivi tunandege nane ,katuletea elimu bure ambapo enzi zetu tulikuwa tunaziita elimu za upe ,katutengenezea barabara sasa na bado anafanya kazi kwanini tusimuite Nyerere mdogo,pia tunapenda kumpongeza mkuu wetu wa wilaya Jerry Muro kwani amesimamia wilaya yetu vyema kuanzia sekta ya elimu,Afya, maji na zinginezo" walisema wazee hao.

Akiongea na wazee hao mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro aliwashukuru wazee hao kwa kupokea wito wake huku akitaja lengo kuwaita ni kusikia changamoto mbalimbali zinazowakabili wazee hao pamoja kuzungumza ,kuangalia namna ya kuzitatua pamoja na kupata ushauri mbalimbali kutoka kwao kwani wazee ni hazina . 

Aliwataka wazee wasipotoshwe na wanasiasa Bali watumie akili zao kupembua ukweli ni upi ,kwani wakiwasikiliza wanasiasa baadhi ni waongo na hawatekelezi yale ambayo wanahaidi kipindi ambacho wanaomba kura ,huku akiwataka wazee kuendelea kuwaasa Vijana na kuwashauri kuendelea kupenda na kuilinda Tanzania yetu.

Aliwahakikishia wazee hao kutatua kero zao zote ambazo wamezitaja kuanzia kero za Vitambulisho vya huduma za matibabu kwa wazee ambapo alisema kuwa kuanzia sasa wazee wote watakao enda katika vituo vya Afya, wapewe huduma bure kwa haraka na at a kama mzee atakuwa amesahau kitambulisho kinachomtambulisha ,au bima ya afya apatiwe huduma kwanza ndio mengine yafuate,huku akitoa maelekezo kwa wakurugenzi wa halmashauri zote mbili kuhakikisha Ndani ya miezi miwili wazee wawe wamepatiwa Vitambulisho vya huduma za Afya .

"Napenda kuwaambia kuanzia leo mzee yeyote akienda hospitalini apatiwe matibabu bure bila kudaiwa chochote na apatiwe dawa zile zote za msingi zilizopendekezwa na katika halmashauri zetu dawa zetu zote zenye msingi zipo Nana napenda kuwaambia mzee yeyote ambaye atanyimwa huduma anipigie aniambie amekosa huduma ili nimchukulie hatua Kali Mtumishi Huyo maana nyie wazee ni hazina " alisema Muro

Aidha aliwahaidi wazee hao kupitia mabaraza yao kuwapatia kiasi cha shilingili milioni tano kwa ajili ya kutunisha mifuko yao ya wazee hao

Naye Mkurugenzi wa halmashauri ya Arusha Wilson Mahela alisema kuwa serikali ya awamu ya tano inawaheshimu sana na kuwajali wazee na ipo tayari kutatua kero zao zote zinazowakabili.
 Mmoja wa mzee akitoa changamoto yake katika kikao cha wazee wa wilaya ya Arumeru kilichoandaliwa na mkuu  wa wilaya hiyo.
 Mkurugenzi wa halmashauri ya Arusha  Wilson Mahela akiongea na wazee hao.
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro  akiongea na wazee  wa halmashauri ya wilaya ya Arumeru wakati alipokutana nao kujadili changamoto zinazo wakabili wazee hao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...