
Waziri wa Madini Mhe.Dotto Biteko akizungumza katika mkutano wa Kupokea Ripoti kutoka kwenye kamati iliyoundwa na Waziri wa Madini Dotto Boteko leo Mirerani.

Mwenyekiti wa Kamati ya Teule iliyoundwa kwaajilivya kutatua migogoro kati ya TML na wachimbaji wadogo Mhandisi Hamis Kamando.

Waziri wa Madini Dotto Biteko kushoto kwake Katibu mkuu wizara ya Madini Profesa Simon Msanjila kimsikiliza Meneja wa Mgodi wa Tanzanite Afrika Wilfred Mushi a(liyevaa shati jeupe)


Mkuu wa mkoa wa Manyara Alexanda Mnyeti akizungumza katika mkutano wa Kupokea Ripoti kutoka kwenye kamati iliyoundwa na Waziri wa Madini Dotto Boteko leo Mirerani.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexanda Mnyeti akisalimiana na Mkurugenzi wa kampuni ya TML Hussein Gonga.
Waziri wa Madini Dotto Boteko akipokea maelekezo kuhusu ujenzi wa Kituo cha ukaguzi wa madini kilichopo Mirerani Mkoani Manyara.
Picha ya jengo la Kituo cha kukagulia madini kikiwa katika hatua za mwisho kumalizika kama kinavyoonekana.Picha zote na Vero Ignatus Michuzi Blog.
Na.Vero Ignatus,Manyara.
WAZIRI wa Madini Mhe.Dotto Bitteko amefuta jumla ya leseni zaidi ya elfu 12 ambapo kati ya leseni 33 elfu zilikuwa zimepewa hati za makosa kwa kutokulipa kodi ya leseni ya mwaka huku kampuni ya TanzaiteOne wanadaiwa dola 98 ambapo kodi hiyo inatosha inatosha kufuta leseni ya uchimbaji
Akipokea ripoti ya migogoro ya mipaka kati ya wachimbaji wadogo na Tanzanite One iliyopo Merereni Mkoani Manyara ambapo kamati hiyo ilibaini makosa 13 ambapo kamati hiyo ni ya tisa kati ya kamati 8 zaawali ambazo zilichunguza mgogoro huo.
Amewataka baadhi ya watu kutokujipa haki kwani yeye kama waziri mwenye dhamana anapimwa kutokana na utendaji wake wa kazi ,hivyo amewataka kupunguza maneno yasiyokuwa na maana ila waacheni watu wafanye kazi kwa ufasaha.
"Hivi leo tuna uparesheni ya watu wanao uza madini kwenye masoko ya nje, mimi haijalishi kuwa wewe ni ndugu yangu au shemaeji yangu, kwani miongoni mwao yup mmoja shemeji yangu,lakini mie ninamwambia kuwa atarudi wakati utaratibu wa serikali ukikamilika"Alisema Biteko
Aliahidi kukaa na kamati yake haraka iwezekanavyo kutoa majibu ya taarifa aliyokabidhiwa na kamati aliyoiteua ya kuchunguza mgogoro huo uliodumu kwa kipindi kirefu.Hata hivyo amewataka waajiri wa wachimbaji wadogo (Apolo) kuwapa stahiki zao kwani muda wa nguvu zao utakapokwisha wao wanabaki bila ya kuwa na thamani yeyote kwa familia na badala yake kuwa mizigo kwaserikali hapo baadae.
Naibu waziri wa madini Stanslaus Nyongo ameipongeza kamati kwa kazi nzuri waliyoifanya huku akioma radhi kwa sintofahamu ambayoilijitokeza
kati ya mbunge Olemilya na Mkuu wa mkoa wa Manyara ambapo awali walionyesha kuzozana wakati wa uwasilishaji wa ripoti hiyo.
Awali akiwasilisha taarifa ya kamati mwenyekiti wa kamati hiyo Mhandisi Hamisi Kamando alisema wamebaini makosa 13 ikiwemo la TanzaniteOne kuwa na leseni ya uchimbaji wa madini ya viwandani huku
wakichimba madini ya vito kinyume cha sheria na kuongeza kuwa leseni hiyo ndio chanzo cha migogoro kwani wamebaini kufanya kazi kwenye kitalu B kwa zaidi ya mita 50 eneo ambalo siyo lao.Mbali na hilo kamati imependekeza mkataba kati ya TanzaniteOne na STAMICO uvunjwe na leseni yake ifutwe kwani ndio chanzo cha migogorona kwamba inafanya kazi kinyume cha sheria.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...