Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Isaac Kamwele akizungumza na wamiliki wa meli Duniani kuhusu namna watakavyofanya kazi nao ili kuongeza ufanisi kwenye bandari ya Dar es Salaam pamoja na kuangalia namna watakavyoweza kuunguza muda wa meli zenye mizigo kukaa bandarini ili kuhudumia meli nyingi wakati wa kikao hicho kilichofanyka katika ukumbi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof Palamagamba Kabudi akizungumza na wamiliki wa meli Duniani kuhusu uhusiano uliopo kati ya Tanzania pamoja na nchi majirani katika ufanyaji wa biashara pamoja na kutoa historia ya Tanzania  kabla na baada ya ukoloni wakati wa kikao ili kuwahamasiha wamiliki hao kuweza kuleta meli zao kwa kutumia Bandari ya Dar es Salaam, Tanga na Mtwara. Kulia ni Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Isaac Kamwele.
Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga akizungumza na wamiliki wa meli pamoja na wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) wakati wa kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wamiliki wa Meli wakiwasilisha changamoto kwa Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Isaac Kamwele wanazozipata pale wanapotumia bandari ya Dar es Salaam wakati wa kikao kilichoandaliwa na Waziri huyo ili kutatua changamoto hizo ikiwemo Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) .
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko(katikati) akifuatilia kwa umakini kikao cha wamiliki wa Meli kilichoitishwa na Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Isaac Kamwele ili kuweza kutatua changamoto wanazozipata katika Bandari ya Dar es Salaam.
Baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), wizara, Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) na wamilii wa meli wakiwa kwenye kikao kilichoitishwa na Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Isaac Kamwele ili kusikiliza changamoto wanazozipata wafanyabishara hao pale wanapotumia Bandari ya Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof Palamagamba Kabudi  akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza kikao cha wamiliki wa meli pamoja na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kilichoandaliwa na Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Isaac Kamwele ili kuweza kutatua changamoto ili kuweza kuingeza ufanisi wa bandari hiyo.
Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Isaac Kamwele akizunguza na waandishi wa habari kuhusu baadhi ya changamoto wanazozipata wamiliki wa Meli kama vile tatizo la mzigo kukaa kwenye maji unakuwa na gharama kubwa  pamoja na kuondoa urasimu wowote kwenye masuala ya uendeshaji wa Bandari ili kuongezeka kwa meli zitazokuwa zinaleta mizogo kwenye bandari hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kukamilika kwa gati nyingine ambayo itaongeza ufanisi wa bandari hiyo mara baada ya kumalizika kwa kikao cha wamiliki wa meli kilichoandaliwa na Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Isaac Kamwele.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko akiwaonesha meli ya kwanza iliyotia naga kwenye gati mpya na kuweza kushusha mbolea wakati wa wamiliki wa meli walipotembelea badari ya Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Isaac Kamwele akizungumza na wamiliki wa meli walipotembelea Bandari ya Dar es Salaam ili kujionea ufanisi wa bandari hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...