Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amepongeza utendaji wa Bodi ya PSPTB na kueleza umuhimu wa kuundwa kwa Bodi hiyo ni pamoja na kusaidia wadau wapate   bidhaa kwa wakati na kulingana na thamani ya pesa zao.

Aliongea hayo wakati alipotembelea banda la PSPTB na kuelezwa majukumu ya Bodi hiyo na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa PSPTB Godfred Mbanyi na hayimaye kukabidhiwa jarida lenye kuonesha kazi mbalimbali zilizofanya na PSPTB na muundo mzima wa Bodi ya wakurugenzi na menejimenti ya PSPTB. 

 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisoma moja ya jarida kwenye banda la bodi ya ununuzi na ugavi(PSPTB) kuhusu  jinsi bodi hiyo inavyofanya kazi wakati wa ufunguzi wa wa Maonesho ya Vyuo vikuu yanayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa bodi ya ununuzi na ugavi(PSPTB) Godfred Mbanyi  
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa bodi ya ununuzi na ugavi(PSPTB) Godfred Mbanyi(katikati) kuhusu mfumo wa usajili na jinsi bodi hiyo inavyofanya kazi wakati wa ufunguzi wa wa Maonesho ya Vyuo vikuu yanayofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...