Makamu wa Pili wa Raiswa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini “B” Nd. Makame Mwadini na Mkuu wa Wilaya hiyo Nd. Rajab Ali Rajab kabla ya kuanza Kikao cha kutathmini hali ya Elimu Wilayani humo.
Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na Walimu Wakuu, Wenyeviti wa Kamati za Skuli, Madiwani Masheha na baadhi ya Maafisa wa Wilaya ya Kaskazini B hapo Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya Kinduni.
Mdau wa Elimu Mwakilishi wa Viti Maalum Mkoa Kaskazini Unguja Mh. Panya Ali Abdulla akitoa mchango katika Kikao hicho kilichosisitiza ushirikiano baina ya washirika wa Elimu Wilayani humo.
Mkurugenzi wa Elimu Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini “B” Maalim Moh’d Juma Makame akitoa ufafanuzi wa mabadiliko ya Mitaala inayowajibikiaWanafunzi kwenda nayo kwa wakati ili kufuzu vyema kwenye Mitihani yao ya Taifa.
Mdau wa Elimu Maalim Muhamed Ali Abduula akihimiza umoja na mshikamano katika mbinu na mikakati ya kuwafinyanga Wanafunzi kufanikiwa katika Mitihani yao.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar {SUZA} Bibi Rehema Abdulrahman akiwakumbusha Walimu kubadilika katika ufundishaji ili kwenda sambamba na mabadiliko ya sayansi na Tekenolojia Duniani.
Mkuu wa Wilaya ya Makaskazini “B” Nd. Rajab Ali Rajab akieleza mfumo utakaotumika katika kuunda Kamati Maalum ya Wilaya itakayosimamia Elimu ndani ya Wilaya hiyo.Picha na – OMPR – ZNZ.









Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...