Na.Khadija seif, Michuzi tv 

KAMPUNI ya Multi Choice Tanzania kupitia King'amuzi Cha dstv wamewahakikishia mashabiki wa soka kuendelea kuwapatia mechi ya ligi kuu maarufu duniani kwa msimu mpya.

Ligi ambazo zitarushwa mubashara kwa lugha ya kiswahili ni Ligi kuu ya Uingereza(EPL), Italia (Serie A), Hispania (La Liga), Liga ya mapingwa Ulaya(UEFA) pamoja na makombe mengine maarufu.

Akizungumza na waandishi wahabari Mkuu wa Masoko wa Kampuni hiyo Ronald Shelukindo amesema pazia la msimu mpya litafunguliwa Agosti 2 kwa mtanange wa ngao ya jamii.

"Msimu huu tutaanza na Ligi ya ngao ya jamii Kati ya Liverpool na kigogo wa Ligi ya Uingereza Manchester City huu utakua mubashara kwa lugha ya nyumbani kiswahili," alisema Shelukindo

Akaongeza kuwa watangazaji wa msimu huu ni Salama Jabir, Edo Kumwembe, Maulid Kitenge, Ibrahim Madoud, Abduli Liongo na Oscar Oscar pia kingamuzi cha DStv unaweza kuunganisha vifaa mbalimbali kama vile Simu, Tablet na Laptop.

Aidha uzinduzi huo ulihudhuriwa na wadua wa soka, wachezaji wastaafu Sekolojo Chambua, Mohmed Hussein na Fikiri Magoso na wasanii mbalimbali Pierre Liquid, Romeo Jonsoni' Dj RJ' na Quickracka.
Mkuu wa Masoko wa kampuni hiyo, Ronald Shelukindo akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa msimu mpya wa soka iliyofanyika katika hotel ya New Africa jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa MultiChoice Tanzania Jacqueline Woiso Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa msimu mpya wa soka iliyofanyika katika hotel ya New Africa jijini Dar es Salaam, kulia ni Mkuu wa Masoko wa kampuni hiyo, Ronald Shelukindo, Kauli Mbiu ya Msimu huu ni SOKA MWANZO MWISHO’
Afisa Masoko na Mawasiliano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania Bi. Shumbana Walwa akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika leo kwenye hoteli ya New Afrika jijini Dar es salaam.
MMoja wa wachezaji wa zamani Sekilojo Chambua akizungumza katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa MultiChoice Tanzania Jacqueline Woiso na Mkuu wa Masoko wa kampuni hiyo, Ronald Shelukindo pamoja na wafanyakazi wengine wakiwa meza kuu wakifurahia jambo katika hafla hiyo.
Meneja Mawasiliano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania Bw. Jonson Mshana akiwa pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo mara baada ya uzinduzi wa msimu mpya wa soka.
Mmoja wa wachambuzi wa soka Ole Mjengwa akizungumza wakati hafla ya uzinduzi wa msimu mpya wa soka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...