Pichani wadau mbalimbali wakipata maendelezo kutoka kwa wataalam wa GST ndani ya Banda la Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) katika maonesho ya Jumuhiya ya nchi za maendeleo kusini mwa Afrika(SADC) yaliombatana na maonesho ya wiki ya viwanda.
Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) , yaendelea kutoa elimu kwa wadau wa sekta ya madini nchini katika maonesho ya wiki ya viwanda yanayoendelea katika mkutano mkuu wa 39 wa Nchi za Jumuhiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).
Moja ya elimu inayotolewa na GST ni juu ya kazi za utafiti wa jiosayansi kwa maana ya jiolojia , jiokemia , jiofikia , miamba na madini nchini ikiwemo madini ya viwandani , madini nakshi (Dimension Stone), elimu nyingine ni juu ya uwepo wa madini ya ujenzi nchini.
Sambamba na elimu hiyo GST ipo na machapisho mbalimbali ya vitabu vya utafiti wa jiosayansi kama vile kitabu cha Madini yapatikanayo Tanzania toleo la nne kitabu hiki kinaelezea uwepo wa madini kuazia ngazi kijiji mpaka taifa.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...