Wananchi wa mkoa wa Arusha na maeneo ya jirani wamehimizwa kutumia fursa ya maonyesho ya 88 yanayoendelea kusajili upya namba zao za simu na kuthibitisha kwa njia ya kibiometria kwani huduma hiyo inapatikana katika maonyesho pamoja na waliopata changamoto ya mawasiliano kwenda katika kupata ufumbuzi.
Akizungumza katika Banda la maonyesho la Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) kanda ya Kaskazini Mkuu wa kanda Hiyo Mhandisi Imelda Salum amesema TCRA ikishirikiana na makampuni ya simu wamehakikisha kuwa huduma hiyo inakuwepo kurahisisha na kusogeza huduma kwa wananchi.
Amesema sambamba na huduma hiyo TCRA pia inatoa elimu ya matumizi bora na salama ya huduma za mawasiliano na kuwataka wananchi wenye matatizo wafike bandani hapo kwa ajili ya ushauri.
Wanafunzi wakipata elimu ya mawasiliano katika banda la TCRA katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini mkoani Arusha
Wananchi wakipata huduma katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini mkoani Arusha.
Wanafunzi na Wananchi wakipata wakipata maelezo katika banda la TCRA katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini mkoani Arusha.
Afisa wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Noah Lalataika akimpa maelezo huduma mwananchi aliyetembelea Banda la TCRA katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini Mkoani Arusha.






Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...