Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Projestus Aloyce Rugazia (pichani) amefariki dunia. 

Mhe. Jaji Rugazia amefariki dunia alfajiri ya kuamkia Agosti 04, 2019 akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa-Muhimbili jijini Dar es Salaam. 

Msiba upo nyumbani kwake Kinondoni- Dar es Salaam, ratiba ya taratibu za kuaga na mazishi itajulikana mapema Agosti 05, 2019. 

Marehemu Jaji Rugazia alizaliwa Agosti 28, 1954 mkoani Kagera, alianza kazi rasmi Januari 01, 1983 kama Hakimu Mkazi. 

Marehemu aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu Machi 28, 2003. Aidha; Marehemu Jaji Rugazia alistaafu rasmi Agosti 28, 2016 akitokea Mahakama Kuu-Divisheni ya Ardhi. 

Mahakama ya Tanzania imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo chake. 

BWANA AMETOA, BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE 


IMETOLEWA NA : 

KITENGO CHA HABARI, ELIMU NA MAWASILIANO, 

MAHAKAMA YA TANZANIA. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...