NA MWAMVUA MWINYI,MAFIA

WATU sita wamenusurika kifo kufuatia ndege ndogo iliyokuwa ikitoka wilayani Mafia ,mkoani Pwani kuelekea Jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa za awali zilizotolewa na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Rufiji ,Onesmo Lyanga zinasema hadi sasa hakuna kifo kilichoripotiwa,zaidi ya watu sita kujeruhiwa.

Lyanga alisema kuwa ndege hiyo ilikuwa ikitoka Mafia kwenda uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere.

“Ndege hiyo ndogo ilianguka ilipokuwa ikitaka kuruka na kurudi chini na kudababisha majeruhi hao ambapo hadi sasa hakuna ripoti ya mtu yoyote aliyefariki dunia,” alifafanua Lyanga.

Alieleza bado jeshi la polisi wako eneo la tukio kukagua na kufuatilia ajali hiyo na taarifa zaidi zitatolewa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...