Na Editha Edward -Tabora
Mamlaka ya Mapato TRA mkoani Tabora imelewa jukumu na Serikali la kuhakikisha inakusanya mapato kiasi cha Shilingi Bilioni 29.3, wakati ambapo Sheria mpya ya ukusanyaji wa mapato imeanza kufanya kazi
Meneja wa TRA mkoa wa Tabora Thomas Masese amesema kulingana na Sheria hiyo itaweza kusaidia ongezeko la kodi ndani ya mkoa huo ukilinganisha na mwaka uliopita na kutoa elimu kwa Wafanyabiashara katika wilaya ya Urambo, Kaliua na Tabora manispaa
" Mwaka uliopita tulikusanya kodi kwa asilimia tisini kulingana na sheria hii itaweza kusaidia ukusanyaji wa mapato katika mkoa wetu zaidi ya asilimia tisini " Amesema masese
Wakizungumza na wafanaya biashara hao baadhi ya wakuu wa Wilaya mkoani humo, akiwemo mkuu wa wilaya ya manispaa ya Tabora Komanya Erick wamewasisitiza Wafanyabiashara umuhimu kwa kulipa kodi pamoja na utunzaji wa kumbukumbu
"Kodi ndiyo roho ya nchi yeyote duniani kodi ndiyo kitu pekee ambayo inawez kukamilisha miradi mbalimbali ya ndani ya nchi kwa hiyo tunachotakiwa tulipe kodi kwa maendeleo ya Taif letu"Amesema Komanya
Kwa upande wao wafanyabiashara wa mkoani Tabora Patrick Chokara na Amina Ally .Wamesema licha ya sheria hiyo kuwa na manufaa kwa Wafanyabiashara lakini bado wana wasiwasi kulingana na wafanyabiashara wengi kutokuwa na Elimu ya Biashara
Aidha Serikali katika mwaka wa fedha 2019 /2020 ilifanya marekebisho ya mfumo wa kodi ikiwemo kurekebisha baadhi ya viwango vya kodi tozo na ada zinazotolewa chini ya sheria mbalimbali pamoja na taratibu za ukusanyaji na usimamizi wa mapato ya Serikali.
Meneja wa TRA mkoani Tabora Thomas masese akizungumza nawa Wafanyabiasha mkoani Tabora.
Pichani ni Wafanyabiasha mbalimbali mkoani Tabora wakimsikiliza meneja wa TRA (pichani Hayupo).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...