Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ally akiangalia shughuli za uzalishaji wa mikanda ya Gypsum unavyofanyika katika kiwanda cha Idetemya wilayani Misungwi jana.Picha na Baltazar Mashaka.
Katibu Mkuu wa CCM Dk. Bashiru Ally, akiwa nje ya jengo la ofisi ya CCM Tawi la Ng'ombe, baada ya kuweka jiwe la msingi, ujenzi ambao umegharimu sh. 8,835,000 ambapo Diwani wa Kata ya Igokelo lilipo tawi hilo Bernad Poly akichangis sh. milioni 2.3, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela na wasaidizi wake sh. milioni 2. Charles Kitwanga (Mbunge) akichangia mabati 80 yanayotakiwa kumalizia jengo hilo.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza Dk. Anthony Diallo (mwenye kofia) akimuongoza Katibu Mkuu wa CCM Dk. Bashiru Ally (kushoto), baada ya kumaliza kukagua ujenzi wa ofisi ya CCM Tawi la Igokelo wilayania Misungwi.
Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ally (kulia) akizungumza na Mbunge wa Misungwi, Charles Kitwanga 'Mawe Matatu' kushoto, kabla ya kuendesha harambee ndogo ya kuchangia ujenzi wa ofisi ya tawi la CCM Ng'ombe,Dk. Bashiru aliahidi kuchangia sh. milioni 2, huku Kitwanga alitoa mabati 80.
Mbunge wa Misungwi Charles Kitwanga 'Mawe Matatu' (kulia) wakiteta jambo na Mwenyekiti wa CCM MKoa wa Mwanza, Dk. Anthony Diallo (kushoto)wakati wa mkutano wa Katibu Mkuu Dk. Bashiru Ally, wilayani Misungwi jana, katikati ni Mjumbe wa NEC mkoani humu, Jamal Abdul Babu. Picha na Baltazar Mashaka
Mlezi wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CCM Dk. Bashiru Ally, akizungumza na wanachama wa CCM na watendaji wa serikali wilayani Misungwi jana.Picha zote na Baltazar Mashaka .


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...