Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT),Prof.Florens Luoga amekutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia kanda ya ya Afrika (Africa Group 1), Bi.Anne Kabagambe ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Gavana Luoga amemwelekeza Bi.Kabagambe hatua mbalimbali ambazo BoT inachukua kuhakikisha kuna ukuaji wa uchumi,kuimarisha sekta ya mabenki,mifumo ya malipo na huduma jumuishi za kifedha.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki Kuu ya Dunia aliipongeza BoT kwa hatua mbalimbali inazochukua kutekeleza sera ya fedha na na kueleza utayari wa Benki ya Dunia kushirikiana katika nyanja mbalimbali za kimaendeleo.

Manaibu Gavana wa BoT, Dkt.Yamungu Kayandabila na Dkt.Benard Kibesse na Mshauri Mwandamizi wa Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji huyo, Bw.Zarau Kibwe, walihudhuria mazungumzo hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...