Na Karama Kenyunko, Michuzi Tv.

CHAMA cha ACT- Wazalendo kupitia bodi yake ya dhamini, wamewasilisha maombi ya kujiunga katika kesi ya kikatiba iliyofunguliwa na mkulima Dezydelius Patrick Mgoya, ambaye anahoji kuwepo kwa kikomo cha urais nchini.

Maombi hayo yamebainishwa leo Septemba 30, 2019 na Jaji Kiongozi wa mahakama hiyo, Dk Eliezer Feleshi, wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutajwa na maelekezo maalumu ya namna ya usikilizwaji wa pingamizi la awali la Seriali dhidi ya kesi ji Kiongozi Dk Feleshi ndiye kiongozi wa jopo la majaji wanaosikiliza kesi hiyo. Wengine katika kesi hiyo ni Dk. Benhajj Masoud na Seif Kulita.

Katika maombi hayo, ACT inayowakilishwa na kampuni ya uwakili ya Law Guards Advocates wamewasilisha maombi hayo chini ya hati ya dharura, wakiomba maombi yao yasikilizwe haraka.

Kufuatia maombi hayo, mahakama imesimamisha usikilizwaji wa kesi ya msingi na kuamua kusikiliza kwanza maombi hayo ya ACT-Wazalendo.

Jaji Feleshi ambae anaongoza jopo la majaji watau wakiwemo Dk. Benhajj Masoud na Seif Kulita amesema, maombi hayo ya ACT- Wazalendo yatasikilizwa na jaji mmoja ambaye atalitaarifu jopo hilo kuhusu uamuzi utakaofikiwa na kesi hiyo sasa itatajwa Oktoba 25 kwa ajili ya maelekezo muhimu.

Wakili wa ACT- Wazalendo, Jebra Kambole ameeleza kuwa maombi ya wateja wake yamepangwa kusikilizwa na jaji Benhajj na kwamba yamepangwa kutajwa kwa mara ya kwanza keshokutwa, Jumatano, Oktoba 2, 2019.

Katika maombi hayo pamoja na mambo mengine, chama hicho kinadai kuwa ikiwa uamuzi wa kesi hiyo utapitishwa bila wao kushirikishwa kitaathirika na kwamba kina haki ya kusikilizwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mkulima huyo mkazi wa Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam, Patrick Dezydelius Mgoya amefungua kesi hiyo Mahakama Kuu, Masjala Kuu dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, akiiomba mahakama hiyo itoe tafsiri sahihi ya ibara ya katiba inayoweka ukomo huo wa urais.

Kwa mujibu wa hati ya madai ya kesi hiyo namba 19 ya mwaka 2019 Mgoya anahoji Ibara ya 40 (2) ya Katiba ambayo inaweka ukomo wa mihula miwili tu ya miaka mitano mitano (10) ya uongozi katika nafasi hiyo ya urais.

Hivyo anaiomba mahakama hiyo itoe tamko na tafsiri ya maana sahihi na athari za masharti ya ibara hiyo.

Pia anaiomba mahakama itoe tafsiri ya maana dhahiri ya masharti ya Ibara ya 42(2) ya Katiba, kwa kuhusianisha na na masharti ya Ibara za 13, 21 na 22 za Katibahiyo.

Vilevile anaiomba mahakama itoe tafsiri ya maana ya Ibara hiyo ya 40(2) kwa kuhusianisha na Ibara ya 39 ya Katiba.

Katika hati yake ya kiapo kinachounga mkono kesi hiyo, Mgoya anadai kuwa lakini Ibara ya 40(2) ya Katiba inaweka ukomo wa muda wa mtu kuchaguliwa kuwa rais, kwamba mtu hawezi kuchaguli zaidi ya mara mbili kushikilia wadhifa wa uraisi

Hivyo anadai kuwa masharti ya ibara hiyo ya 40(2) yanakiuka haki za kikatiba za Ibara za 13, 21 na 22(2) za Katiba hiyohiyo kwa kutoa mihula miwili tu ya raia kuchaguliwa kuwa rais kwa ukomo wa miaka 10 tu.

Mgoya anadai kuwa ukomo uliowekwa chini ya Ibara ya 40(2) ya Katiba yanakinzana na haki ya kikatiba ya uhuru wa kushiriki katika shughuli za umma kwa kuchagua au kuchaguliwa kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na usawa mbele ya sheria chini ya Ibara ya 21 na 13

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...