Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
Wakala wa Usambazaji wa mashine ya kumwaga Lami ya Dynapac Paver Kampuni ya Apollo Heavy Equipment wamekabidhi mashine ya kumwaga lami iliyotengenezwa nchini Ujerumani.

Kampuni hiyo leo wamekabidhi mtambo huo ukiwa ni wa pili kuingia nchini ndani ya mwaka.mmoja.

Mashine hiyo ya kumwaga lami kutoka kampuni ya Dynapac ya nchini Sweden imekabidhiwa kwa Kampuni ya Ukandarasi ya Mayanga inayojihusisha na uuzaji wa vifaa mbalimbali.

Akizungumza baada ya kukabidhi mtambo huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Appolo, Ruben Mwambene amesema wamekuwa mawakala wa kuleta vifaa vyote vinavyotengenezwa na kampuni ya Dynapac kwa miaka mitatu sasa. Amesema, mashine hiyo ya kumwaga lami ni wa pili ndani ya mwaka mmoja na wamekuwa wanauza mashine mpya na vipuli vyake. Mwambene amesema, "Ni miaka mitatu tumekuw mawakala wa kuleta mitambo na vipuli vyake kutoka kampuni ya Dynapac inayopatikana nchini Sweden ambao pia wamesambaa kwenye nchi tofauti duniani"

"Tumekabidhi mashine hii kwa kampuni ya Ukandarasi Mayanga ajili ya ujenzi wa barabara za Musoma na imani kubwa kila kitu kitaenda sawa,"

Amesema, mashine hizo zina ubora mkubwa na imara. Na wameweza kuikabidhi kwa kampuni ya Ukandarasi ya Mayanga kwa ajili ya ujenzi wa barabara za Musoma.
 MKURUGENZI Mtendaji wa kampuni ya Apollo Heavy Equipment Ltd, Reuben Mwambene, akikabidhi mashine ya kuwekea lami kwa mwakilishi wa kampuni ya Ukandarasi ya Mayanga, Arif Salim (kushoto), Dar es Salaam leo kwa ajili ya ujenzi wa barabara za Musoma.
MKURUGENZI Mtendaji wa kampuni ya Apollo Heavy Equipment Ltd, Reuben Mwambene (kulia), akimpa maelezo kuhusu mashine ya kuwekea lami kwa mwakilishi wa kampuni ya Ukandarasi ya Mayanga, Arif Salim (kushoto), wakati akimkabidhi mashine hiyo, Dar es Salaam leo kwa ajili ya ujenzi wa barabara za Musoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...