Wakati wa uzinduzi wa wiki ya usikilizwaji,utoaji huduma na utatuzi wa kero za wananchi wilayani Korogwe, Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mhe. Kissa G. Kasongwa amekemea watumishi wote wa Serikali ambao wanatabia ya kutowasikiliza na kuwahudumia wananchi vizuri pale wanapokwenda katiaka ofisi zao na kuongeza kuwa wananchi ndio mabosi wa wahusika wote serikalini. 

Alisema kama yeye Mkuu wa Wilaya wa Korogwe anatoa kiti chake ofisini na kukaa nje katika eneo la kuegeshea magari ili kuwasikiliza wananchi kwa unyenyekevu wote.

Mhe. Kasongwa alitoa rai kwa watumishi wote wa idara na taasisi, kuwa waende wawasikilize wananchi na kuto watolea maneno mabaya na kuwahimiza kufanya kazi kwa bidii na weredi ili kufikisha azma ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kutaka kuwafikia wananchi wanyonge.

Taasisi mbalimbali zitatoa huduma katika wiki hii, ikiwa ni pamoja na Mfuko wa Fidia kwa wafanyakazi (WCF) , PSSSF, NHIF, NSSF, NIDA, RITA, PCCB, TRA, Damu Salama, Jeshi la zima moto, Benki mbalimbali ikiwa ni pamoja na NMB na CRDB, Kampuni za Simu ikiwa ni pamoja na Halotel, TTCL, Mawakili wanaotoa msaada wa kisheria pamoja na taasisi mbalimbali
Mhe. Kissa G. Kasongwa Mkuu wa Wilaya ya Korogwe akizindua rasmi wiki ya usikilizwaji,utoaji huduma na utatuzi wa kero za wananchi wilayani hapo kuanzia tarehe 21 - 24 Septemba 2019, katika viwanja vya ofisi ya Mkuu wa Wilaya Korogwe tarehe 21.09.2019
Viongozi wa Dini wakifungua kwa maombi wiki ya usikilizwaji,utoaji huduma na utatuzi wa kero za wananchi 
Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe Bi. Rehema Bwasi akitoa maelezo ya chimbuko la wiki ya usikilizwaji,utoaji huduma na utatuzi wa kero za wananchi katika Wilaya hiyo.
Mbunge wa Korogwe mjini Mhe. Mary Chatanda akitoa sakamu zake kwa wananchi wakati wa uzinduzi wa wiki ya usikilizwaji,utoaji huduma na utatuzi wa kero za wananchi wilayani Korogwe.
Mbunge wa Korogwe Vijijini Mhe. Timotheo Mzava akitoa salamu zake kwa wananchi wakati wa uzinduzi wa wiki ya usikilizwaji,utoaji huduma na utatuzi wa kero za wananchi wilayani Korogwe.
Mwenyekiti wa CCM Korogwe vijijini Bw. Nassoro Malingumu akitoa salamu zake wakati wa wiki ya usikilizwaji,utoaji huduma na utatuzi wa kero za wananchi wilayani Korogwe
Mwenyekiti wa CCM Korogwe mjini Bw. Immanuel Chale akitoa salamu zake wakati wa wiki ya usikilizwaji,utoaji huduma na utatuzi wa kero za wananchi wilayani Korogwe
Wananchi mbalimbali wakiwa katika uzinduzi wa wiki ya usikilizwaji,utoaji huduma na utatuzi wa kero za wananchi 
Waananchi mbalimbali kutoka Wilayani Korogwe wakipata huduma wakati wa wiki ya usikilizwaji,utoaji huduma na utatuzi wa kero za wananchi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...