Meneja wa Ufundi wa Bodi ya Maziwa, Deogratius Mlay akitoa maelezo kuhusiana na maadhimisho ya unywaji wa maziwa jijini Dar es Salaam.
Afisa Mauzo wa Tanga Fresh, Protas Kimario akitoa maelezo namna ya Tanga Fresh inavyhamasisha unywaji wa maziwa katika shule na umhimu wa maziwa hayo katika shule ya Msingi Ali Hassan Mwinyi.
Afisa Lishe wa Manispaa ya Kinondoni Emiliana, Daud akizungumza na wanafunzi katika maadhimisho ya unywaji wa maziwa shuleni duniani ambapo Tanga Fresh imegawa maziwa katika shule za msingi saba za manispaa hiyo.
Wanafunzi wakipewa maelezo katika wiki ya unywaji wa maziwa.
Wanafunzi wakigaiwa maziwa katika maadhimisho ya unywaji wa maziwa.
Wanafunzi wakinywa maziwa katika wiki ya unywaji wa maziwa
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
SHULE za Msingi Saba katika jiji la Dar es Salaam zimeadhimisha maadhimishisho ya wiki ya unjwaji wa maziwa shule ikiwa ni kujenga watoto kuwa na afya bora.
Akizungumza na wanafunzi wa shule ya Msingi Ali Hassan Mwinyi Meneja wa Ufundi wa Bodi ya Maziwa Deogratius Mlay amesema kuwa unywaji wa maziwa unatakiwa kuwa endelevu kwani ni shule 25 ndio zina program za unywaji wa maziwa shuleni.
Amesema kuwa bodi ya maziwa imekuwa na mikakati ya kuhakikisha jamii inatengeneza mazingira ya unjwaji wa maziwa pamoja na bidhaa za maziwa katika kujenga afya bora na kuweza kuzalisha mali kwa maendeleo ya taifa.
Aidha amesema kuwa bodi na utaratibu wa kwenda katika mabaraza ya shule katika kuweka kipaumbele cha unjyaji wa maziwa shuleni kwa kutoa fedha kwa watoto kwa ajili ya maziwa.
Amesema kuwa mtu anatakiwa kunywa maziwa lita 200 kwa mwaka lakini unjwaji huo uko chini hivyo jamii ijenge mazingira ya kunywa maziwa hayo .
Kampuni ya Maziwa ya Tanga Fresh ndio imekuwa ikitoa pakiti moja kwa kila mtoto ikiwa ni kuadhimisha unywaji wa maziwa shule saba hizo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...