Muonekano wa jengo la Mahakama ya Mwanzo Magoma.
Muonekano wa ndani wa jengo la Mahakama ya Mwanzo Magoma.






Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Tanga, Bw. Ahmed Ng’eni,(aliyeinama) ambaye amemwakilisha Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania,akigagua sehemu ya kukaa maabusu ya Mahakama ya Mwanzo Magoma, iliyopo Korogwe mkoani Tanga, wakati wa makabidhiano ya ujenzi wa Mahakama hiyo yaliyofanyika Septemba 19, mwaka huu. Makabidhiano hayo yalihusisha Mkandarasi – SUMA JKT Kanda ya Kaskazini, Mshitiri – Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania aliyewakilishwa na Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Tanga, Mshauri elekezi wa Mradi – Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mkoa wa Tanga pamoja na Mshauri mdogo wa umeme na Mitambo (TEMESA) Mkoa wa Tanga.


Mkadiliaji Majenzi (QS) Yassin Khatib (mwenye shati nyeupe) kutoka TBA, akielezea jambo wakati wa makabidhiano hayo.


Mtendaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Tanga,Bw. Ahmed N’geni (kulia wa tatu) na Kapteni E. P. Mapunda, ambaye ni Mwakilishi wa Meneja wa Kanda SUMA JKT wakitia saini makabidhiano hayo na wa pili kushoto ni Mkadiliaji Majenzi (QS) Yassin Khatib (mwenye shati nyeupe) kutoka TBA. (Kulia wa pili) ni Afisa Utumishi wa Mahakama Kuu Tanga, Bw. Faridi Mnyamike, akifuatiwa na Mlinzi wa Mahakama ya Mwanzo Magoma, Bw. Miraji Sufian.


Mtendaji Mkuu wa Mahakama Kuu Tanga, Bw. Ahmed N’geni(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wengine, ambao wapili kulia ni Kaimu Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Tanga, Mhe. Cassian Matembele na wa kwanza kulia ni Afisa Utumishi wa Mahakama Kuu Tanga, Bw. Faridi Mnyamike. Kushoto ni Afisa Tawala wa Mahakama ya Wilaya Korogwe, Bw. Emmauel Machimo akifuatiwa na Kapteni E. P. Mapunda.
(Picha na Amina Ahmad – Tanga)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...