Mratibu wa Shirika lisilokua la kiserikali la INFOY ,Laurent Sabuni

Na  Woinde Shizza Michuzi Tv, Arusha
MRATIBU wa Shirika lisilokua la kiserikali la infoy Laurent amewataka Vijana wa Kitanzania  kuchangamkia fursa ya kuongeza thamani mazao na kuyafungasha katika viwango vya ubora wa hali ya juu ili yaweze kukubalika katika masoko ya ndani ya nje

Sabuni amesema hayo katika mkutano wa wadau kutoka asasi za kiraia zinazojishughulisha na vijana ambazo zinafadhiliwa na The Foundation for Civil Society  ambapo amesema kuwa  wamekua wakitoa mafunzo ya usindikaji wa bidhaa za chakula hususan lishe pamoja namna ya kuzifungasha bidhaa hizo ili kupanua wigo wa fursa kwa vijana.

"Vijana licha ya kujishughulisha na ujasiriamali pia wanapaswa kuongeza thamani ya mazao ya nafaka kama mahindi,ngano na hata mazao ya mifugo kuyachakata na kuyafungasha vizuri na kuyafikisha sokoni yakiwa katika hali nzuri ya kuvutia masoko ya ndani na nje" Alisema Sabuni

Kwa upande wao vijana Fransisca Wilson  amesema kuwa tayari wameanza kutengeneza unga wa lishe kwa kutumia nafaka hivyo kuwasaidia kuinua kipato chao na kuchangia maendeleo katika jamii zao.

Leonard Paulo amesema kuwa mwamko wa vijana katika kuongeza thamani umeongezeka huku changamoto kubwa ikiwa ni mtaji wa kuanzia biashara zao na kununua mazao kwa kulima pamoja na mashine za kuchakata mazao na kutengeneza bidhaa.

 Afisa Vijana na Maendeleo Jiji la Arusha Hanifa Ramadhani alisema kuwa  vijana hao wanapaswa kusindika bidhaa za nafaka na kutengeneza bidhaa mbalimbali ambazo zinahitajika katika jamii badala ya kuacha mazao ya wakulima wakati mwingine yamekua yakiharibika kwa kukosa soko Na pia kutokuongezwa thamani jukumu ambalo inapaswa lifanywe na vijana. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...