WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amezitaka Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuwa kuwa na mipango, sera, viwango na mifumo ya pamoja ya kisheria itakayorahisha utoaji wa huduma za usafirishaji wa bidhaa na kukuza biashara ndani ya Ukanda huo.
Akifungua Mkutano wa Mawaziri wa Jumuiya hiyo wanaosimamia sekta za Tehama, Habari, Uchukuzi na Hali ya Hewa leo Alhamisi (Septemba 19, 2019) Waziri Mkuu Majaliwa aliwataka Mawaziri hao kutumia mkutano kuandaa mapendekezo ya suluhisho la changamoto ya nnjia bora za kuimarisha mtandao wa biashara ndani ya sadc.
Majaliwa alisema Tanzania kwa upande wake imekuwa mstari wa mbele katika nja wanachama wa SADC katika kuboresha miundombinu ya usafirishaji ikiwemo kuboresha bandari ya Dar es Salaam ambayo kwa sasa imekuwa ikihudumia  Nchi mbalimbali za Jumuiya ya SADC ikiwemo Jamhuri ya Kidemokrasia ya  Kongo, Malawi na Zambia pamoja na Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Aliongeza kuwa Tanzania pia imeendelea na ujenzi na reli ya kisasa inayojengwa katika Ukanda wa kati pamoja na ujenzi wa reli ya Tazara inayonganisha Tanzania na  Zambia, na kutaja juhudi hizo ni moja ya mikakati ya Tanzania ya kuhakikisha inaimarisha mtandao wa biashara ndani ya Jumuiya hiyo.
“Katika Ukanda wa reli ya Tazara kwa sasa tumeweza kuongeza kiwango cha usafirishaji kutoka tani 88,000 mwaka 2014/2015 hadi kufikia tani 220,000 mwaka 2017/2018 pamoja pia na kujenga Meli 2 za mizigo katika Ziwa Nyasa zenye uwezo wa kubeba tani 200” alisema Majaliwa
Akizungumzia kuhusu Maendeleo ya Sekta ya Tehama katika Ukanda wa SADC, Majaliwa alisema Nchi hizo hazina budi kufikia malengo yaliyowekwa katika Mkutano Windohoek Nchini Namibia mwaka 2018 wa kuhakikisha kuwa kunawepo na Intaneti yenye kasi kwa ajili ya kurahisisha shughuli za kibiashara na utoaji huduma kwa wananchi ifikapo mwaka 2023.
Aliongeza kuwa kwa mujibu wa taarifa ya  Shirika la Mawasiliano  Duniani (ITU) zinaonesha kuwa matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasliano katika Nchi za SADC imekuwa na kufikia asiliami 22.3 ikilinganisha na kiwango cha dunia ambacho ni asilimia 51, na hivyo kuwa katika kiwango cha juu ikilinganishwa na kiwango kilichowepo katika miaka ya 2000.
Akifafanua zaidi Waziri Mkuu Majaliwa aliwataka Mawaziri hao kuweka mkazo katika kujadili kiwango cha matumizi na umuhimu wa kuunganisha Intaneti ili kuweza kuongeza kasi ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wananchi wa Jumuiya hiyo.
Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe alisema kutokana na Nchi za SADC kuwa na changamoto zinazoshabihiana katika masuala ya hali ya hewa, Tehama, Uchukuzi na Habari, Mkutano wa Mawaziri hao umepanga kuweka mikakati ya pamoja itakayosaidia kuimarisha ustawi wa wananchi wake.
Aidha aliongeza kuwa Mkutano huo umehudhuriwa na Mawaziri wa Nchi 8 za Jumuiya hiyo ikiwemo Angola, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji, Zambia, Afrika Kusini, Lesotho, Zimbambwe, Tanzania ambapo Mawaziri hao katika Mkutano wao wa siku mbili wanatarajia kujadili masuala mbalimbali ikiwemo maazimio yaliyopitishwa katika Mkutano Mkuu wa 39 wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya hiyo uliofanyika Agosti 17-18 mwaka huu.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Miundombinu na Huduma wa SADC, Rosemary Mokoena alisema Mkutano huo wa Mawaziri unatarajia kujadili masuala mbalimbali ambayo ni muhimu katika utekelezaji wa Mipango Mkakati mbalimbali iliyopangwa kutekelezwa na jumuiya hiyo katika kuimarisha mifumo ya biashara na huduma mbalimbali ndani ya SADC.
 NI MUHIMU KUWEKEZA KWENYE TEHAMA

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema ili kuleta maendeleo endelevu ya viwanda, kuongeza biashara na kutengeneza ajira, nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) zinapaswa kuwekeza katika uunganishaji na uwianishaji wa viwango mbalimbali vya TEHAMA. 

Amesema hatua hiyo itasaidia kutatua changamoto za maendeleo ya miundombinu na muingiliano wa mawasiliano nje ya mipaka ya nchi na kikanda. “Changamoto hizo zinajumuisha maunganisho ya njia kuu za mawasiliano kati ya nchi jirani, kuyafanya mawasiliano ya kikanda yabaki ndani ya kanda, maunganisho ya kuvuka mipaka ya nchi, upangaji wa bei pamoja na uwianishaji wa viwango.”

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Alhamisi, Septemba 19, 2019) wakati akifungua Mkutano wa Pamoja wa Mawaziri wa SADC wa sekta ya TEHAMA,  uchukuzi na hali ya hewa pamoja na kongamano maalumu la Mawaziri, unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu amesema kwa kipindi hiki, nchi wanachama zinapaswa kuhakikisha kuwa utekelezaji unalenga katika teknolojia zinazochipukia kwenye utoaji wa huduma za posta sambamba na kuanzisha huduma na bidhaa mpya ambazo zitakidhi mahitaji ya sasa ya wateja na kuhamasisha biashara mtandao. 

“Katika kufanikisha hili, ni muhimu kufanya tathmini ya utekelezaji wa Mkakati wa Posta wa SADC wa mwaka 2017-2020 ambao uliridhiwa mwezi Septemba, 2017.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema ili kufikia mtangamano wa kikanda kuhusua miundombinu ya usafiri na usafirishaji, mkutano huo unapaswa kuzungumza namna gani nchi wanachama zinaweza kuwianisha sera, viwango, mifumo ya sheria katika maeneo ya barabara, reli, usafiri wa anga, usafiri wa majini, pamoja na hali ya hewa. 

Waziri Mkuu amesema kuna haja ya kuboresha miundombinu muhimu ya usafirishaji, utaratibu wa ugavi na usafirishaji wa vitu na huduma pamoja na kuwezesha kutoa mizigo kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine ndani ya kanda. “Hivyo, nawaomba katika mkutano wenu mjadili maeneo haya na kuja na mapendekezo ya suluhisho ili kutatua vikwazo mbalimbali.”

“Tanzania imeweza kuboresha miundombinu ya bandari pamoja na mifumo ya uendeshaji ili kusaidia nchi za SADC ambazo hazipakani na bahari nazo ni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Jamhuri ya Zambia, Jamhuri ya Malawi pamoja na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki za Jamhuri za Uganda, Rwanda na Burundi.” 

Waziri Mkuu amesema kuwa nchi wanachama wa SADC zinapaswa kuboresha mifumo ya reli kwa kuzingatia Mpango Mkakati Elekezi wa Maendeleo wa Kikanda wa mwaka 2015-2063 pamoja na Mpango Kamambe wa Maendeleo ya Miundombinu wa Kikanda wa mwaka 2019-2023. 

Amesema kati ya miradi mikubwa inayotekelezwa hapa Tanzania, ni pamoja na ujenzi wa reli ya kisasa ya mwendo kasi inayojengwa katika ukanda wa kati pamoja na ukarabati wa Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) ambayo inaunganisha nchi wanachama wa SADC. “Hivyo, katika ukarabati uliofanyika wa TAZARA, umeongeza uwezo wa reli hiyo kusafirisha mizigo kutoka tani 88,000 mwaka 2014/2015 hadi tani 220,000 mwaka 2017/2018.”

Mkutano huo unahudhuriwa na Mawaziri wa Sekta ya TEHAMA, Habari, Uchukuzi na Hali ya Hewa kutoka nchi za Angola (4), Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (2), Msumbiji (1) Zambia (3), Afrika Kusini (2), Lethoto (1), Zimbabwe (2) na Tanzania inawakilishwa na Mawaziri watano na Naibu Waziri Mmoja, akiwemo Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe ambaye ndiye Mwenyekiti wa Mkutano huo.

 
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mawaziri wa SADC wa Sekta ya TEHAMA, Habari, Uchukuzi na Hali ya Hewa wanakutana kwa siku mbili kuanzia leo Septemba 19-20, 2019 jijini Dar es Salaam. Picha zote na Matokeo Chanya+. Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG. 
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhandisi Isack Kamwelwe akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mawaziri wa SADC wa Sekta ya TEHAMA, Habari, Uchukuzi na Hali ya Hewa wanakutana kuanzia leo Septemba 19-20, 2019 jijini Dar es Salaam. Nae Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amesema mkutano huo umewakutanisha wataalamu wa tehama, hali ya hema, uchukuzi na mawasiliano kutoka nchi wanachama pamoja na wakuu wa taasisi na mashirika pamoja na viongozi waliopo katika sekta binafsi nchi za SADC. Amesema katika majadiliano wote kwa pamoja wanazo changamoto mbalimbali wanazoshabihiana katika hali ya hewa, miundombinu mbalimbali ambayo inarudisha nyuma nchi kujikomboa kiuchumi na kuwa wana mjadala wa pamoja katika kuzileta nchi kiuchumi kwa manufaa ya wananchi wa ukanda huu. “Kipindi cha asubuhi tumeshaanza na tumeendelea na mjadala wajumbe walileta hoja mbalimbali kushuhghulikia reli, majanga na hali ya hewa, manufaa ya teknolojia ya habari na mawasiliano katika kuboresha uchumi na maisha ya wana SADC. “Aidha wataalamu kutoka sekta za kibenki maendeleo ya Afrika na Benki ya Maendeleo ya Afrika Kusini wameelezea uwezo wao katika kusaidia ujenzi na uboreshaji wa miundombinu katika sadc, lakini pia maeneo mengine yaliyoangaziwa ni pamoja na ushirikishwaji wa wanawake na sekta binafsi,” amesema Kamwelwe.
Mkurugenzi wa Miundombinu wa SADC, Mapolao Mokoena amesema mkutano huo utaweza kusaidia uelewa wa watendaji wa Serikali kujua njia ya kupita katika kuifanya jumuiya ifikie malengo yake hasa katika miundombinu.
Mawaziri wa SADC wa Sekta ya TEHAMA, Habari, Uchukuzi na Hali ya Hewa wanakutana kwa siku mbili kuanzia leo Septemba 19-20, 2019 jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa akiwa na Mkurugenzi wa Miundombinu wa SADC, Mapolao Mokoena (kushoto).
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhandisi Isack Kamwelwe (wa kwanza kushoto) akiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (katikati) pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Sekta ya Uchukuzi Bw. Leonard Chamriho.
Mawaziri wa SADC wa Sekta ya TEHAMA, Habari, Uchukuzi na Hali ya Hewa wanakutana kwa siku mbili kuanzia leo Septemba 19-20, 2019 jijini Dar es Salaam. Meza kuu.
Meza kuu wakiendelea na majadiliano.
Mawaziri wa SADC wa Sekta ya TEHAMA, Habari, Uchukuzi na Hali ya Hewa wakiuliza maswali wakati wa majadiliano.
Majadiliano yakiendelea...
Mawaziri wa SADC wa Sekta ya TEHAMA, Habari, Uchukuzi na Hali ya Hewa wanakutana kwa siku mbili kuanzia leo Septemba 19-20, 2019 jijini Dar es Salaam.
Cathbert Kajuna 19:11 (2 hours ago) to amichuzi, othmanmichuzi, me ....TUMIE HII KUNA MAREKEBISHO YA JINA LA WAZIRI MKUU.... WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AWASISISTIZA MAWAZIRI WA SADC KUSIMAMIA MAENDELEO YA TEKNOLOJIA
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Mawaziri wa SADC wa Sekta ya TEHAMA, Habari, Uchukuzi na Hali ya Hewa wanakutana kwa siku mbili kuanzia leo Septemba 19-20, 2019 jijini Dar es Salaam. Picha zote na Matokeo Chanya+. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa akiwa na Mkurugenzi wa Miundombinu wa SADC, Mapolao Mokoena (kushoto).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...