Waziri wa Mifugo na  Uvuvi Luhaga Mpina amewataka wafugaji kuongeza uzalishaji wa maziwa nchini ili kuchochea uwekezaji katika Tasnia ya Maziwa.

Hayo amesema jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano na  waandishi wa habari kuelekea siku ya unywaji maziwa shuleni Duniani itakayoadhimishwa Septemba 25 mwaka huu  mkoani Iringa.

Mpina amesema kuwa ni mikakati ya serikali kuhakikisha kuwa uzalishaji wa maziwa unaongezeka kutoka lita bilioni 2.7 hadi kufika lita bilioni 7 kwa mwaka ifikapo 2020.

Amesema kuwa  malengo ya serikali ifikapo mwaka 2025 kila shule ya msingi iwe na  programu za kunywa maziwa shuleni na kila mtanzania awe anakunywa angalau  lita 100 kwa mwaka.

Kwa sasa kuna shule 25 tu ambazo zinatekeleza Programu ya unywaji maziwa shuleni na  kunufaisha jumla ya wanafunzi16.849 kwenye wilaya za Njombe, Mbeya na Wangingo'mbe.
Programu hizi zinaendeshwa kwa ushirikiano na  Mamlaka za Serikali za Mitaa, Viwanda vya kusindika maziwa, wazazi na wafadhili mbalimbali.

Waziri Mpina ametoa pia rai kwa wananchi kunywa maziwa na bidhaa za maziwa ili kuchochea maendeleo ya Tasnia ya Maziwa.

Maadhimisho ya Siku ya Unywaji Maziwa shuleni yanatarajiwa kufanyika mkoani Iringa uwanja wa Samora. Kauli Mbiu ya Maadhimisho haya ni Glasi moja ya maziwa kila siku kwa afya na  Elimu bora.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Kupanga Mpina akizungumza na waandishi habari kuhusiana maadhimisho ya Siku ya unywaji wa Maziwa yatakayofanyika mkoani Iringa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...