Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akisisitiza jambo wakati akizungumza na watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji katika ukumbi wa ofisi ndogo za wizara ya kilimo Jijini Dodoma, leo tarehe 13 Septemba 2019. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akisisitiza jambo wakati akizungumza na watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji katika ukumbi wa ofisi ndogo za wizara ya kilimo Jijini Dodoma, leo tarehe 13 Septemba 2019.
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba (Mb) akizungumza wakati wakati wa kikao kazi kilichoitishwa na Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga kukutana na watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji katika ukumbi wa ofisi ndogo za wizara ya kilimo Jijini Dodoma, leo tarehe 13 Septemba 2019. 


Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameipa wiki moja Tume ya Taifa ya umwagiliaji kutengeneza mikakati ya kutengeneza mabwawa ya kukinga maji ya mvua ili kuwasaidia wakulima kuwezesha kilimo cha umwagiliaji kukua.

Mhe Hasunga ameyasema leo tarehe 13 Septemba 2019 katika ukumbi wa ofisi ndogo za wizara ya kilimo Jijini Dodoma alipokuwa akizungumza kwenye kikao kazi na watumishi wa Tume huyo. 

Waziri Hasunga amesema kuwa wizara hiyo ina matarajio ya kutumia fursa ya mradi mradi wa umeme wa maporomoko ya maji ya Mto Rufiji (RHPP) utakaozalisha megawati 2115, kea ajili ya kilimo cha umwagiliaji ambapo inatajwa kuwa kuna zaidi ya Hecta 150,000 zinazofaa kea ajili ya umwagiliaji.

Mhe Hasunga amewataka watendaji hao wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kuhakikisha kuwa wanampatia mipango na mkakati wa namna gani baada ya umeme kuzalishwa katika eneo lile, yale maji yatatumika yote katika umwagiliaji na hecta zote zile zianze uzalishaji.

‘’Ninawapa wiki moja hakuna muda mwingine wa kufanya hivyo kwa sababu niliwapa mienzi minne hamjafanya hivyo’’ Alisema Mhe Hasunga.Aidha, Waziri Hasunga ametoa siku tatu kumpatia taarifa za utendaji kazi wa miradi ya umwagiliaji katika mikoa minne yaani Tabora, Katavi, Rukwa, na Songwe iwapo kuna miradi inayofanya kazi na isiyofanya kazi. 

Kilimo cha umwagiliaji kimekuwa kikisisitizwa na serikali kwani ni kilimo kisichotegemea mvua hivyo kuwa na matarajio ya kuvuna mazao kwa wingi.

Umwagiliaji ni mtindo wa kilimo wa kupeleka maji kwa mimea shambani pasipo mvua ya kutosha, hutumiwa katika maeneo yabisi au wakati mvua ni kidogo. Katika nchi baridi unatumiwa pia kwa kusudi la kulinda mazao dhidi ya jalidi.

Ni kilimo ambacho kinasaidia sana, kwa mfano nchi ya Misri tangu zamani inategemea mto Naili katika shughuli zake za umwagiliaji wa mazao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...