Meneja wa Kampuni ya Uchimbaji madini ya Lindi Jumbo Paul Shauri akionesha michoro ya muonekano wa eneo la mgodi wa madini aina ya uno (Graphite) wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika masuala ya Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki pamoja na Naibu Waziri ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt.Angeline Mabula.

Naibu Waziri ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt.Angeline Mabula akizungumza jambo wakati wa kikao cha majumuisho cha ziara ya kutembelea miradi ya uwekezaji katika Wilaya ya Ruangwa mkoni Lindi pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika masuala ya Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki (aliyekaa kulia) kilichofanyika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Bw. Hashim Mgandilwa akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa kikao hicho cha Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika masuala ya Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki pamoja na Naibu Waziri ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt.Angeline Mabula katika ofisi zake Mkoani Lindi.

Katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Ruangwa Bw. Barnabans Essau akisalimia wakati wa kikao hicho.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika masuala ya Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki pamoja na Naibu Waziri ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt.Angelline Mabula wakiwa katika ziara ya kukagua eneo lililotengwa kwa ajili ya uchimbaji wa madini aina ya uno (Graphite) lililopo Wilayani Ruangwa Lindi Septemba 27, 2019.
(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...