Katika kuboresha huduma zake kwa wateja, Benki ya Exim Tanzania leo imezindua huduma mpya zinazolenga kuhamasisha wateja wake na jamii kwa ujumla kuhusu uwepo wa akaunti zake mpya tatu zinazofahamika kama Akaunti ya ‘Haba na Haba', Akaunti ya ‘Haba na Haba Plus’ pamoja na Akaunti ya ‘Mzalendo’ zote zikilenga kuwawezesha wateja hao kuhifadhi fedha bila makato ya mwezi kwa matumizi ya kuweka akiba na kwa shughuli za kila siku.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma mpya kwa wateja jijini Dar es salaam mapema leo, Mkuu wa Idara ya Amana wa Benki ya Exim Tanzania, Bi Agnes Kaganda alisema kuwa huduma hizo zinalenga wateja wote  ikiwemo wenye kipato cha chini, kati na kipato kikubwa.

"Akaunti hizi za Haba na Haba zinalenga kukidhi mahitaji ya wateja ambao wanahitaji kuhifadhi fedha zao kwa matumizi ya siku zijazo. Huduma zote zimelenga kutatua changamoto ya ukosefu wa namna iliyo bora ya kuhifadhi fedha miongoni mwa watanzania walio wengi bila kuwa na akiba isiyopungua pitia makato ya kila mwezi,’’ alisema.

Aidha, akifafanua kuhusu akaunti ya Haba na Haba, Bi Agnes Kaganda alisema inawalenga watu wenye nia ya kuweka akiba kwa ajili ya malengo ya baadae huku akitaja faida zinazombatana na ufunguaji wa akaunti hiyo kuwa ni pamoja na kunufaika na kiwango cha juu cha riba, hakuna makato ya mwezi na huduma ya haraka katika matawi yote ya benki hiyo,

“Pia inatoa fursa ya kuweka kiwango chochote cha akiba kwa wateja aidha kila mwezi au kwa muda wowote ambao wateja wataona ina manufaa kwao katika kutimiza malengo yao, Wateja wataweza dunduliza akiba zao kupitia simu za mikononi kutoka Mpesa/Tigopesa/Airtel money/Zantel kwenda kwenye akaunti ya Haba na Haba.’’ alitaja


Ili kufungua akaunti hiyo Bi Agnes Kaganda alisema mteja anapaswa kuwa na picha mbili sampuli ya hati ya kusafiria (passport size), nakala moja ya kitambulisho ambacho kinaweza kuwa hati ya kusafiria, kitambulisho cha kitaifa, au leseni ya udereva, Uthibitisho wa makazi au kibali cha makazi kwa raia wa kigeni na barua kutoka kwa serikali ya mtaa pamoja na fedha kiasi cha Tsh 50,000 kama kiasi cha kuanzia.

Akizungumza kuhusiana na akaunti ya Haba na Haba Plus, Bi Agnes Kaganda alisema inawalenga watu wenye kipato cha juu ambao pia kupitia akaunti hiyo wataweza kunufaika na viwango vikubwa vya riba.

 “ Akaunti hii pia inalenga kukidhi mahitaji ya wateja ambao wanahitaji kuhifadhi fedha zao kwa matumizi ya siku zijazo.’’ Alisema huku akitaja faida zitokanazo na ufunguaji wa akaunti hizo kuwa ni pamoja na kunufaika na kiwango cha juu cha riba na huduma ya haraka katika matawi yote ya benki hiyo.
“Pia inatoa fursa ya kuweka kiwango chochote cha akiba kwa wateja aidha kila mwezi au kwa muda wowote ambao wateja wataona ina manufaa kwao katika kutimiza malengo yao, Kunufaika na riba kubwa jinsi akiba yako inavoongezeka ikiwa sambamba na huduma zilizoongezwa thamani kutoka kwa Mameneja wanaohusika na mahusiano ya wateja. Wateja wataweza dunduliza akiba zao kupitia simu za mikononi kutoka Mpesa/Tigopesa/Airtel money/Zantel kwenda kwenye akaunti ya Haba na Haba.’’ alitaja
“Pia ili kufungua akaunti hii mteja anapaswa kuwa na picha mbili sampuli ya hati ya kusafiria (passport size), nakala moja ya kitambulisho ambacho kinaweza kuwa hati ya kusafiria, kitambulisho cha kitaifa, au leseni ya udereva, Uthibitisho wa makazi au kibali cha makazi kwa raia wa kigeni na barua kutoka kwa serikali ya mtaa pamoja na fedha kiasi cha Tsh 10,000,000 kama kiasi cha kuanzia.,’’ alitaja

Alitaja akaunti ya tatu kuwa ni Mzalendo akaunti ambayo itawawezesha wateja kupata huduma ya kufanya mihamala ya kila siku kupitia benki hiyo masaa 24 na siku saba za wiki bila kukatwa malipo ya kila mwezi  na pamoja na kupatiwa ATM kadi ya malipo bure.

Bi Agnes Kaganda alizitaja faida za akaunti hiyo kuwa ni pamoja na kutoa fursa kwa mmiliki wake kuweza kuindesha bila kuwekewa kiwango cha chini cha salio, haina ada ya uendeshaji,kupatiwa kadi ya malipo bure pamoja na manunuzi kwenye maduka yote yenye huduma ya POS (merchant Point of Sale) bila gharama yoyote.


‘Pia ili kufungua akaunti hii mteja anapaswa kuwa na picha mbili sampuli ya hati ya kusafiria (passport size), nakala moja ya kitambulisho ambacho kinaweza kuwa hati ya kusafiria, kitambulisho cha kitaifa, au leseni ya udereva, Uthibitisho wa makazi au kibali cha makazi kwa raia wa kigeni na barua kutoka kwa serikali ya mtaa’’ alisema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...