Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu (Mawasiliano), Dkt. Jim Yonazi (katikati mbele waliokaa), akiwa katika picha ya pamoja na washindi wa shindano hilo, walimu, wazazi pamoja na wageni wengine waliohudhuria kwenye hafla hiyo.

Mgeni rasmi, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mawasiliano), Dkt. Jim Yonazi, akimkabidhi zawadi mshindi wa kwanza wa shindano la uandishi wa barua Kimataifa nchini, Joan John Erasto (wapili kushoto), wa Shule ya Sekondari Binza, mkoani Simiyu. Hafla ya maadhimisho ya miaka 145 ya Siku ya Posta Duniani imefanyika jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni mwalimu wa shule hiyo, Japhet Kilela.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Elia Madulesi akitoa maelezo katika hafla hiyo. Kulia ni Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mawasiliano), Dkt. Jim Yonazi. Wapili kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika, Dkt. Haruni Kondo.

Baadhi ya Maofisa wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakifuatilia hotuba mbalimbali katika maadhimisho hayo. 

Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika, Mwanaisha Said, akizungumza katika hafla ya maadhimisho hayo. 

Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu-Mawasiliano, Dkt. Jim Yonazi akimkabidhi zawadi mshindi wa tatu wa uandishi wa barua, Hasnein Rizwan kutoka shule ya Sekondari ya Almuntazir Boys Seminary ya jijini Dar es Salaam.

Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu (Mawasiliano), Dkt. Jim Yonazi akimkabidhi cheti mshindi wa pili wa shindano hilo, Grace Kahimba wa Shule ya Msingi ya St. Ann’s ya Morogoro. Kulia ni Kaimu Postamasta Mkuu Mwanaisha Said na wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika, Dkt. Haruni Kondo. 

Mshindi wa kwanza nchini katika shindano la Kimataifa la uandishi wa barua, Joan John Erasto, akiisoma barua yake iliyompatia ushindi wakati wa hafla hiyo.

Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania, Dkt. Haruni Kondo akizungumza katika maadhimisho hayo, leo jijini.Kaimu Postamasta Mkuu Mwanaisha Said, akimkaribisha Mgeni rasmi, Naibu Katibu Mkuu (Mawasiliano), Dkt. Jim Yonazi (katikati), kuzungumza katika hafla hayo.





Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu (Mawasiliano), Dkt. Yonazi akizungumza katika maadhimisho hayo.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Uwakala wa Usafiri wa ndege nchini (MAUFU), Maua Katandula, ambao ni mmoja wa wadhamini wa shindano la kimataifa la Uandishi wa Barua nchini, akizungumza katika maadhimisho hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...