AGIZO la Rais Magufuli la kutaka kurejeshwa kwa fedha za Chuo cha Ualimu cha Mongere kilichopo wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro cha kiasi  shilingi million 76 .9 zilizo tafunwa na  aliyekua Mhasibu wa Chuo Cha uwalimu Sarafina Mbwambo na Melkizedek Mchau karani Wa Miamala Wa ELCT ND Sacco's Zimezaa Matunda .  

Watuhumiwa hao wameanza kurejesha  fedha kiasi cha Shilingi Million  54 .8 kati ya fedha kiasi cha shilingi Million 76.9 walio zitumia kupitia  Miamala hewa.

Akipokea Malipo hayo Mara baada ya kutoa wiki mbili fedha hizo kurejeshwa katika Account ya Chuo, Mkuu Wa Wilaya Lengai Ole Sabaya amesema kwamba Fedha Hizo zililipwa na wazazi kwa lengo la wanafunzi kupata Elimu ya kufundisha kozi ya Ualimu na ndipo watumishi hao kujichotea fedha hizo kutumia Account hewa.

Amesema kutokana na watumishi hao kuchota fedha hizo bila huruma wakijua kwamba wazazi wa wanafunzi waliofika chuoni hapo kupata elimu ni watoto wa maskini alitoa wiki mbili fedha hizo kurudishwa katika Account ya Chuo na wanafunzi kuendelea na Masomo. 

Fedha hizo zilileta Mgogoro Mkubwa baina ya uongozi cha chuo pamoja na wazazi Mara baada ya wanafunzi kuingiwa hofu ya kurudi Nyumbani kwa kukosa masomo na ndipo mkuu wa wilaya kuingilia kati na kutoa maagizo ya kukamatwa kwa Muhasibu pamoja na karani wa Miamala hewa.

Sabaya amezitaja taasisi zingine zilizo tafuna fedha hizo ni pamoja na  benki ya Crdb wilani Hai taasisi ya ELCT ND pamoja na chuo cha Ualimu Mongare kwa uzembe wa kuacha kufanya ukaguzi wa mahesabu kwa mwaka mzima Chuoni hapo kiasi cha shilingi million 36.9 

Mkurugenzi wa Chuo hicho  Joseph Mongare Msaki akisoma taharifa ya urejeshwa Fedha amesema kwamba fedha hizo zimeingizwa katika account ya Chuo Mara baada ya utapeli uliofanyika na mhasibu kwa kushirikiana  na wakala wa Sacco's. 

Joseph amesema kwa mujibu wa Maagizo ya Rais kuhagiza fedha hizo kurejeshwa Mara moja katika accounti ya Chuo ndipo kupitia  mkuu wa wilaya kutoa amri ya wiki mbili fedha hizo ziwe zimerejeshwa chuoni.

Mkurugenzi amemshukuru Mkuu wa wilaya pamoja na Rais John Pombe Magufuli kwa fedha hizo kurejeshwa na wanafunzi kuendelea na masomo yao kama hapo awali.

Mkuu wa wilaya Lengai Ole Sabaya toka kukabidhiwa wilaya Hai Amekua mkombozi mkubwa kwa wananchi wa wilaya hiyo kwa kuondoa changamoto ya ubadhirifu wa Mali za umma pamoja na kutatua migogoro ya Ardhi .

CRDB wameomba kuzilipa kwa utaratibu wao ili kumaliza changamoto hiyo jambo ambalo amewakubalia.

Aidha amewataka wanachuo hao pamoja na taasisi zilizo husika katika upotevu wa fedha hizo kuacha uhasama badala yake washirikiane kwakua tatizo limesha malizika.

"Hakuna sababu ya kuchukiana na hizi taasisi tunashukuru Mungu tumemaliza hilo pamoja na Kumshukuru Rais Magufuli kwa kuingilia katika 
 Wanafunzi wa Chuo cha Ualimu cha Mongere kilichopo wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro wakiwa na mabango ya kushukuru Rais.
Mkurugenzi wa Chuo hicho  Joseph Mongare Msaki  akizungumza  Mbele ya Mkuu wa Wilaya 

Mkuu wa wilaya ya hai Lengai Ole Sabaya akionyesha risiti za malipo ya baadhi ya aliekuwa muhasibu wa chuo hicho kwa wanafunzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...