Umoja wa Watanzania Ujerumani UTU e.V umefanya mkutano mkuu wa uchaguzi mjini Aschaffenburg Ujerumani jumamosi 28.09.19. Katika uchaguzi huo watanzania wanaoishi ujerumani walichagua viongozi wapya, nafasi ya mwenyekiti alichaguliwa Mwl. Bi Upendo Vanessa Lymo kuwa mwenyekiti wa UTU e.V, baada ya mwenyekiti mstaafu Bw. Mfundo Peter Mfundo kukataa kugombea nafasi hio, ambayo amekaa kwa muda wa miaka 9, na kukitumikia chama hicho kwa muda wote huo, hata hivyo kamati ilimuomba achukue nafasi ya heshima kuwa mwanakamati, mshauri, mlezi wa UTU e.V na kiongozi muandamizi katika shughuli za UTU e.V

Watanzania wanaoishi ujerumani waliwachagua viongozi wafuatao.

Mwenyekiti: Mwl. Bi Upendo Vanessa Lymo

Makamo Mwenyekiti: Bw. Malumbo Salim Malumbo

Katibu: Bi. Petrida Karch

Muweka hazina: Bw. Mngoya Lukuta

Wanakamati:
Bw. Mfundo Peter Mfundo
Bw. Ebrahim Makunja (aka Kamanda Ras Makunja)
Bw. Sudi Mnette

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...