Umoja wa Watanzania Ujerumani UTU e.V umefanya mkutano mkuu wa
uchaguzi mjini Aschaffenburg Ujerumani jumamosi 28.09.19. Katika
uchaguzi huo watanzania wanaoishi ujerumani walichagua viongozi wapya,
nafasi ya mwenyekiti alichaguliwa Mwl. Bi Upendo Vanessa Lymo kuwa
mwenyekiti wa UTU e.V, baada ya mwenyekiti mstaafu Bw. Mfundo Peter
Mfundo kukataa kugombea nafasi hio, ambayo amekaa kwa muda wa miaka 9,
na kukitumikia chama hicho kwa muda wote huo, hata hivyo kamati
ilimuomba achukue nafasi ya heshima kuwa mwanakamati, mshauri, mlezi
wa UTU e.V na kiongozi muandamizi katika shughuli za UTU e.V
Watanzania wanaoishi ujerumani waliwachagua viongozi wafuatao.
Mwenyekiti: Mwl. Bi Upendo Vanessa Lymo
Makamo Mwenyekiti: Bw. Malumbo Salim Malumbo
Katibu: Bi. Petrida Karch
Muweka hazina: Bw. Mngoya Lukuta
Wanakamati:
Bw. Mfundo Peter Mfundo
Bw. Ebrahim Makunja (aka Kamanda Ras Makunja)
Bw. Sudi Mnette
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...