Mama Shujaa wa chakula kutoka Shirika la Oxfam, Stella Masulya akimuelekeza Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi namna ya anavyohofadhi samaki wake kwa kutumia moshi na anavyoandaa dagaa kwa njia ya asili katika maonesho ya kuadhimisha siku ya chakula duniani yanayoadhimishwa kitaifa mkoani Singida.
 Dkt.Nchimbi akisaini katika kitabu cha wageni katika banda la Oxfam kwenye maonesho hayo.
 Mama Shujaa wa chakula kutoka Arusha, Elinuru Moses akimuelezea Dkt. Nchimbi umuhimu wa kutumia vyakula asilia na namna ya kuvihifadhi.
 Wakina mama Shujaa wa chakula kutoka mikoa mbalimbali walioshiriki maadhimisho ya siku ya chakula duniani wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi.
 Dkt.Nchimbi akipokea zawadi ya viazi lishe vinavyozalishwa na wakulima wadogo wadogo kutoka Mbongwe.
 Mama Shujaa wa chakula kutoka mkoani Mtwara akimuuzia vikapu Dkt. Nchimbi alivyotengeneza kama mjasiriamali mdogo ili kukuza kipato cha familia yake.
Mama Shujaa wa chakula, Elinuru Moses akimuelekeza Dkt. Nchimbi umuhimu wa chakula asilia  katika kuboresha afya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...