Mkufunzi na Mkuu wa Idara ya Ufundi ya JKA/WF-­‐Tanzania kitaifa, pia Mwenyekiti wa Tanzania Shotokan-­‐Ryu Karate-­‐Do Association (TASHOKA) Abdallah Kambi Sensei  amefariki dunia.

Kambi Sensei aliyeingia madarakani tarehe 27 Julai 2019, amefikwa na umautio leo alfajiri katika hospital kuu ya Taifa Muhimbili, alipokua amelazwa kufuatia kusumbuliwa na kifua na tumbo, tangu mwezi August.

Mwenyekiti, JKA/WF-­‐Tanzania Jerome G. Mhagama, amethibitisha kutokea kwa msiba huo, na ameeleza taratibu za maziko ya Kambi Sensei aambaye alijiunga na JKA/WF-­‐Tanzania mwaka 2009 na kuwa mwanafamilia hai wa JKA mpaka umauti unamkuta.
 
Katika hatua nyingine Mhagama ameeleza taarifa nyingine za msiba wa mdau huyo wa mchezo wa Karate, huku wakitarajia majibu wa kikao cha familia ya marehemu.

Ndani ya JKA Kambi Sensei alikuwa mmoja wa Wakufunzi tegemezi mwenye Black Belt 4th Dan-­‐JKA, pia alikuwa na JKA International Licence yenye viwango vya Instructor class C, Judge class D & Examiner class D.
Bwana ametoa, Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe.
Alale mahali pema peponi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...