Sasa TECNO imewapa tena wateja wake nafasi ya kurahia ladha mpya ya simu janja na hii kutokana na ujio wa simu mpya ya TECNO Spark 4 yenye sifa malukuki na kwa bei nzuri.

Akizungumza na vyombo vya habari wakati wa uzinduzi wa TECNO Spark 4 uliofanyika katika duka jipya la TECNO ‘TECNO Smart Hub Kariakoo’ manager wa masoko wa kampuni ya TECNO, Bwana William Motta alisema, “teknolojia ya AI iliyopo ndani ya TECNO SPARK 4 imebeba uwezo mkubwa wenye kuzipa support kamera tatu za nyuma za TECNO Spark 4 kwa picha nzuri na videos zenye ubora. 

William Motta amevieleza vyombo vya habari kuwa TECNO Spark 4 imekuja na sifa zifuatazo Kasi ya mtandao wa 4G, Kamera tatu za nyuma, GB 32 za memory na kioo cha nchi 6.52 super full-view. 

Wakati huo, Mkuu wa idara ya kitengo cha bidhaa wa kampuni ya TIGO Mkumbo Mnyonga alisema, “pindi unaponunua simu ya TECNO Spark 4 basi hapo hapo utazawadiwa na ofay a GB 18 kutoka tigo.uzinduzi wa simu hii mpya unaenda sambamba na ofa ya GB 18 kutoka tigo”. 

Mkumbo Mnyonga “lengo letu ni kuhakikisha jamii ya kitanzania inahamia katika mfumo mpya wa kijital. Na hiyo ndio sababu ya kampuni ya TIGO kushirikiana na TECNO ili kulifikia dhumuni lakuongeza wimbi la watumiaji smartphone nchini”.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...