Mkurugenzi mtendaji wa benki ya NIC Tanzania Limited Margaret Karume, amewaasa wanafunzi wa shule ya sekondari Loyola kujifunza kwa kuzingatia mtizamo mpana wa kidunia ili kuendana na mfumo wa sasa wa kielimu wa kidunia unaohitaji wahitimu wenye uwezo mkubwa wa kuelewa mambo na matatizo mbali mbali na kisha kuyatafutia suluhisho.

Karume aliyekuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 21 ya shule hiyo alitoa wito huo, sambamba na kukabidhi mchango wa magodoro 100 kwa ajili ya kuboresha mazingira wanayoishi wanafunzi wa shule hiyo.

Mkurugenzi huyo pia aliwaambia wanafuzi wa Loyola kuwa ili kuendana na dunia ya sasa, wanatakiwa kufanya jitihada binafsi za kutafuta maarifa na ujuzi na siyo tu kutegemea kile wanachofundishwa na waalimu wao darasani  na kusisitiza kuwa bado wana safari ndefu.

“Elimu mliyoipata bado ni ya hatua za mwanzo tu, hasa ukizingatia kukua kwa utandawazi. Kutokana na mabadiliko makubwa yanayoenda sambamba na ukuaji wa haraka wa Sayansi na Teknalojia yanayomgusa kila mtu na katika kila nyanja ya maisha, sote tutalazimika kuendelea form 6 kujifunza mambo mapya hadi mwisho wa maisha yetu,” alisema

Karume aliwaambia wahitimu hao watarajiwa kwamba ni wajibu wao kuendelea kujifunza mbinu mpya za kuyakabiliana na maisha na pia kujijengea uwezo wa kujiajiri pindi watakapomaliza elimu ya juu

Elimu mliyopata na ambayo mtaendelea kuipata itafungua maisha yenu na ya jamii nzima ikiwa ni pamoja na familia zenu na watoto wenu. Elimu hii pia itawapa uwezo wa kiuchumi, itawapa uwezo wa kuwa na sauti, mtaongea, mtasikika na kusikilizwa, pia itawajengea heshima katika jamii na kuwapa uwezo wa kuchangia mambo mbali mbali katika maisha. 

Aliwataka kuiga mifano ya wanafunzi waliosoma shuleni hapo na ambao wamefanikiwa kimaisha baadhi yao wakiwa ndani na wengine nje ya nchi

Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule hiyo Padri Obwanda Meyo, SJ alimuhakikishia mgeni rasmi kuwa wanafunzi wake wamejiandaa vizuri kwa ajiili ya mitihani ya mwisho na hivyo watafanya vizuri 
Mkurugenzi mtendaji wa benki ya NIC Tanzania Limited, Margaret Karume (kushoto) akiwa ni mgeni rasmi wa sherehe ya wahitimu wa kidato cha nne wa shule ya sekondari Loyola akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi  milioni 4.7/- kwa mkuu wa shule hiyo Father Ubwanda Meyo jana, ikiwa ni sehemu ya mchango wa benki ya NIC kwa ajili ya kununulia magodoro 100 yatakayotumika kwenye mabweni ya wasichana wa  shule hiyo.
Mkurugenzi mtendaji wa benki ya NIC Tanzania Limited Margaret Karume akizungumza na wageni waalikwa , wanafunzi na walimu wa shule ya sekondari Loyola waliohudhuria kwenye mahafali ya wanafunzi wa kidato cha nne shule hiyo jana jijini Dar es salaam
Mkurugenzi mtendaji wa benki ya NIC Tanzania Limited, Margaret Karume (wa pili kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa shule ya sekondari Loyola, Padri Obwanda Meyo (wa tatu kulia), mwakilishi wa wazazi watoto wa kidato cha nne, Joseph Tadayo (kulia), Brigitte Asenga na Annah Lupembe (kushoto) ambaye ni meneja wa tawi la NIC Kariakoo.
Mkurugenzi mtendaji wa benki ya NIC Tanzania Limited Margaret Karume akifurahi na wanafunzi wahitimu wa kidato cha nne shule ya sekondari Loyola.
Mkurugenzi mtendaji wa benki ya NIC Tanzania Limited, Margaret Karume (wa pili kulia mbele) akiwa kwenye picha ya pamoja na wahitimu wa kidato cha nne wa shule ya sekondari Loyola, Mkuu wa Shule Padri Obwanda (aliyebeba mtoto), Mwakilishi wa wazazi, Joseph Tadayo , Mwenyekiti wa PTA Luyola, Brigitte Asenge na Meneja wa Tawi la NIC Kariakoo, Annah Lupembe (mwisho kushoto)
Mkurugenzi mtendaji wa benki ya NIC Tanzania Limited, Margaret Karume akiwa na kikombe alichopewa zawadi na uongozi wa shule ya sekondari Loyola.











Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...