Mafundi wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) Jacob Ezekiel(kushoto) na  Ramadhan Sammata(kulia) wakisaidiana kukata bomba kwa ajili ya kuunga kwenye bomba litakalokuwa linahudumia eneo la Salasala Kilimahewa Juu.
 Mafundi wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA)  Jacob Ezekiel(kushoto) na  Ramadhan Sammata(kulia) wakiunga bomba kwenye moja ya bomba kubwa la maji la bomba kwa ajili kusambaza maji kwenye eneo la Salasala Kilimahewa Juu eneo lililokuwa na ukosefu wa maji ya DAWASA.
Meneja wa DAWASA Mkoa wa Kihuduma Tegeta Ole Philemon  akitoa maelezo kwa Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) Everlasting Lyaro alipokuwa wanashuhudia ufungwaji wa bomba kubwa la maji ya DAWASA yatakayoweza kuhudumia eneo la Salasala Kilimahewa Juu jijini Dar es Salaam.

Mafundi wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) wakitandaza mabomba ya inchi 6  kwa ajili ya kusambaza maji kwenye eneo la Salasala Kilimahewa Juu kwa takribani kilometa 1.5 katika eneo hilo.
Muonekano wa bomba  la inchi sita la Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) likiwa tayari limeishaunganishwa kwenye bomba kubwa na kutandazwa kwa takribani kilometa 1.5
na kufunguliwa kwa ajili ya kuanza kusambaza maji katika eneo la Salasala Kilimahewa  Juu lililokuwa na changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama.
Maji yakitoka kwenye bomba kubwa la inchi 6 eneo la Salasala Kilimahewa Juu mara baada ya kufunguliwa kwa bomba la Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) kwa ajili ya kusambaza maji kwa wananchi wa eneo hilo.
Baadhi ya wananchi wa Salasala Kilimahewa Juu wakichota maji ya Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) mara baada ya maji hayo kufika katika eneo hilo leo jioni kwa ajili ya kuwahudumia wananchi hao waliokuwa wanapata changamoto ya maji ya DAWASA.
Mkazi wa Salasala Kilimahewa Juu Seleman Issa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu upatikanaji wa maji wa DAWASA katika eneo hilo pamoja na kutoa shukrani kwa Mamlaka hiyo kuweza kuwafikia wananchi hao.
Meneja wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) Mkoa wa Kihuduma Tegeta Ole Philemon akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Mamlaka hiyo ilivyojipanga kwenye usambazaji wa maji katika eneo la Salasala Kilimahewa Juu ambalo lililokuwa na tatizo kubwa la upatikanaji wa maji safi na salama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...