Mkuu wa Magereza Mkoani Arusha, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Anderson
Kamtiaro(kulia) akimuonesha Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP
Phaustine Kasike(kushoto) shamba la maharage ambalo limelimwa kwa
kutumia Kilimo cha umwagiliaji Gereza Arusha.
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike(wa pili toka kulia) akitoa maelekezo kwa Mkuu wa Magereza Mkoani Arusha, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Anderson Kamtiaro(kulia)alipokagua Shamba la mahindi kabla ya kuendelea na ziara ya kikazi Mkoani Manyara leo Novemba 16, 2019(Picha zote na Jeshi la Magereza).
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike (kushoto) akizungumza na Mkuu wa Magereza Mkoa wa Manyara, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Lipina Lyimo(katikati) pamoja na Kamishna Msaidizi wa Magereza, Masoud Kimolo(kulia) muda mfupi alipowasili leo Novemba 16, 2019 Mkoani humo. CGP Kasike yupo mkoani Manyara kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kukagua magereza yote ya Mkoa huo na kuzungumza na Maafisa na askari wa Jeshi hilo.
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike akisalimiana na Maafisa wa Magereza Mkoani Manyara mara baada ya kuwasili Gereza Babati kwa ziara yake ya kikazi leo Novemba 16, 2019.
Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini - CGP Phaustine Kasike(meza kuu) akiongoza kikao kazi na Maafisa wa Magereza Mkoani Manyara kabla ya kufanya Baraza la Wafungwa na mahabusu wa Gereza Babati.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...