*Ni baada ya video kusambaa mtandaoni akionesha mtu akitishwa kwa bastola

*Waziri asema hata kiwembe nacho ni silaha,marufuku kumtisha nacho mtu

Na Said Mwishehe, Michuzi Globu ya jamii

BAADA ya kuwepo picha ya video mtandaoni inayoonesha kuna mtu ameshika silaha aina ya bastola akimtisha mtu mwingine, Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola amesema ni kosa kisheria kwa anayemiliki silaha kutaka kuitumia kinyume na sheria na atakayekamatwa atachukuliwa hatua kwani hakuna aliyekuwa juu ya sheria.

Akizungumza leo Novemba 2,2019 jijini Dar es Salaam ,Waziri Lugola amesema ni kosa kisheria kutumia silaha kumtisha mtu au kutaka kumdhuru nayo ." Kwetu sisi wembe,kisu,upinde na aina nyingine ya silaha ni marufuku kumtisha nayo mtu.

"Ipo sheria ya kumiliki silaha, kuitumia na namna ya kuihifadhi.Hivyo kwa wanaomiliki silaha za moto lazima waheshimu sheria ,ni vema Watanzania wote wakawa makini na matumizi ya silaha,'amesema Waziri Lugola.

Hata hivyo amesema kuna mkakati unaandaliwa kupitia Kampuni ya Jeshi la Polisi watatoa mafunzo kwa watu wote wanaomiliki silaha za moto ili kuhakikisha wanazitumia kwa matumizi sahihi na mafunzo hayo yanaweza kutolewa kwa gharama ndogo ya fedha.

"Kila anayemiliki silaha lazima apewe mafunzo ya matumizi bora ya silaha. Hiyo itasaidia kuwakumbusha silaha inahifadhiwa vipi na inatumika vipi.Hata sisi Polisi tumekuwa na utaratibu wa kwenda mafunzo ya mara kwa mara.

"Ambapo huko pia tunakumbushana kuhusu matumizi ya silaha,hivyo lazima na raia ambao wanamiliki silaha wapate mafunzo,"amesema na kuongeza mafunzo hayo yatahusu na ulengaji shabaha.
Hata hivyo amesema sheria ya kumiliki silaha ya moto iko wazi,hivyo yoyote ambaye atakiuka atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria,"amesema Waziri Lugola.

Wakati huo huo amesema katika ziara yake ya kikazi ambayo ameifanya katika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi ameona kazi zinavyofanyika kwa weledi,umakini  na ujuzi huku akisifu namna askari Polisi wanavyotekeleza majukumu yao ya kila siku na kwamba wanastahili pongezi.

Akiwa katika ziara hiyo amepata nafasi ya kuona kazi zinazofanywa na jeshi hilo katika Kitengo cha kuzuia uhalifu mtandaoni ambapo amesema kuna mambo ambayo wamekubaliana ili kufanikisha utendaji kazi.Hata hivyo amesema Polisi wamefanikiwa Kudhibiti matukio ya uhalifu yakiwemo ya wizi mtandaoni .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...