Na Said Mwishehe,Michuzi Globu ya jamii
WAZIRI
wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola amesema siku za mtu anayejiita Kigogo
anayetumia mtandao wa kijamii na hasa Twitter kutukana,kukejeli na
kuikashfu Serikali ya Awamu ya Tano anatakiwa kufahamu siku zake
zinahesabika.
Kwa muda
sasa mtu anayejiita Kigogo2014 amekuwa akitumia mtandao wa kijamii kutoa
taarifa mbalimbali ambazo nyingi zimekuwa zikilalamikiwa na nyingine
zimekuwa zikisababisha mjadala mtaani na mitandaoni kiasi cha baadhi ya
Watanzania kuhoji huyo Kigogo ndio nani,maana haijafahamika kwa jina
zaidi ya kutumia sura kama ya mwanamuziki maarufu wa Marekani Jay Z
ingawa alichokifanya ni kuuurefusha mdomo.
Waziri
Lugola ameyasema hayo leo Novemba 2,mwaka 2019 jijini Dar es Salaam
wakati anazungumzia utendaji kazi wa Jeshi la Polisi nchini ambapo
ameeleza kuridhishwa na utendaji kazi wa jeshi hilo chini ya uongozi wa
Mkuu wa Jeshi la Polisi ,IGP Simon Sirro.
Hata
hivyo waandishi walitaka kufahamu hatua ambazo zinachukuliwa
kukabiliana na baadhi ya watu wenye kutumia mitandao ya kijamii kutoa
lugha za kukejeli,kashfa,kuzusha na dhihaka dhidi ya wengine na hasa
Kigogo2014, ambapo Waziri Ligola amesema kila mtu anafahamu kalenda
inavyohesabiwa ,hivyo Kigogo atambue siku zake zinahesabika na siku si
nyingi atpatikana.
"
Huyo anayejiita Kigogo afahamu kwamba siku zake zinahesabika , ni kama
vile kuhesabu kalenda unaanza moja hadi 31 ,hivyo tutampata tu, "amesema
Waziri wakati akijibu swali kuhusu mtu huyo na kuongeza Watanzania
wanatakiwa kutumia mitandao vizuri na sio kuitumia kwa ajili ya
kupotosha, kuchonganisha au kutukana wengine kwani sheria itachukua
mkondo wake.
Mbali ya
kuzumzungumzia Kigogo, Waziri Lugola ameeleza kutokana na utendaji wa
Wizara ya Mambo ya Ndani na Jeshi la Polisi chini ya Serikali ya Awamu
ya Tano ya Rais Dk.John Magufuli, usalama wa raia na mali zao umeimarika
na hata matukio ya ujambazi yamepungua kwa asilimia kubwa .
Amesema
kuwa Jeshi la Polisi liko imara wakati wote,hivyo amesema wenye tabia
ya kujihusisha na uhalifu watambue kuwa hawako salama na wasithubutu
kutenda uhalifu kwani watakamatwa na watakaokuwa wabishi kwa Kupambana
na Polisi watashughulikiwa.
Pia
amesema kuna majambazi ambao wamekuwa wakifanya ujambazi na kisha
kukimbilia Mkoa wa Kigoma na Kagera, hata hivyo ameeleza Polisi
wameizingira Mikoa hiyo na hivyo majambazi walioko huko muda
wowote watakuwa mikononi mwa jeshi hilo.
Kuhusu
vitendo vya rushwa, Waziri huyo amesema kwa sehemu kubwa rushwa
imepungua lakini ametoa rai kwa kila Mtanzania kuchukia rushwa kwani
hakuna rushwa kama hakuna anaetoa,hivyo mtoa rushwa na mpokea rushwa wote
ni wakosefu mbele ya sheria.
Pia
amezungumzia wa watu kutoa malalamika iwapo watakuwa nayo dhidi ya
Jeshi la Polisi lakini ni vema wakafuata utaratibu kwa kuonana na wakuu
wa vituo vya Polisi na wakaona hawajaridhika wanakwenda kwa wakubwa
zaidi na hata kwa IGP au Wizara ya Mambo ya Ndani.
Amesema
kwa kufanya hivyo anaamini malalamiko dhidi ya Polisi kama yapo badi
yatapata ufumbuzi kwani kuendelea kulalamika bila kufuata utaratibu huo
inaweza kuonekana kama majungu.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhe. Kangi Lugola akifafanua jambo mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) leo Novemba 2,2019 jijini Dar es Salaam,kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo suala la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa,Uhalifu na matumizi mabaya ya silaha na mitandao ya kijamii.
Waziri wa Mambo ya Ndani,Mhe. Kangi Lugola akizungumza na Waandishi wa Habari leo jijini Dar kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo suala la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa,Uhalifu na matumizi mabaya ya silaha na mitandao ya kijamii.Pichani kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Meja Jenerali Jacob Kingu na kushoto ni Mkuu wa Jeshi la Polisi ,IGP Simon Sirro.Picha na Michuzi JR.(MMG).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...