KATIKA shamra shamra za maafali ya 13 ya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) ambayo yatafanyika Disemba 12 mwaka huu, wamendaa maonyesho maalumu ya teknolojia mbalimbali za TEHAMA ambapo pamoja na mambo mengine huduma mbalimbali kwa wananchi zitatolewa ikiwa ni pamoja na kutengenezewa simu pamoja na kompyuta zao.

Mhadhili Msaidizi wa DIT, Daudi Mboma anasema Taasisi hiyo imeandaa maonyesho maalum ya Tehama ambayo yapo chini ya mradi wa Escrip unaofadhiliwa na Benki ya Dunia.

Amesema mradi huo utaanzishwa katika Kampasi ya Dar es Salaam ambapo wataanzisha kituo cha ICT ambayo itakuwa ya kikanda itakayojikita hasa katika usalama wa mitandao.

"Tumeandaa baadhi za wabunifu wanafunzi hapa kwenye Taasisi na wengine ambao wameanzia hapa kwetu na sasa wanajitegemea wamefanikiwa kuanzisha kampuni zao, watakua hapa kuanzia leo hadi siku ya mahafali wakitoa huduma ya kutengeneza kompyuta na simu bure," anasema Mboma.

Karuma Nicholas ni Mwanafunzi aliyesoma katika Taasisi hiyo na ni mmiliki wa kampuni ya Testlimit, anasema elimu inayotolewa DIT ni ya kipekee kwani wanafundisha zaidi kwa vitendo Jambo lililomuwezesha kufanya kazi nyingi za TEHAMA.

Wananchi wanaalikwa katika viwanja vya Taasisi hiyo kutembelea maonesho hayo kujifunza pamoja na kupata huduma bure ya kutengenezewa simu pamoja na komputa zao.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...