Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Nchini, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Fortunatus Muslim akizungumza na madereva wa mabasi yanayokwenda mikoani. 
 
Kamanda Muslim amewataka madereva kuwa waangalifu katika kuhakikisha usalama wa abiria hasa katika kipindi hiki cha mwisho wa mwaka kutokana na uzoefu wa huko nyuma kwamba kipindi kama hiki hutokea ajali nyingi. 
 
Muslim pia aliwataka madereva kuzingatia suala la afya na kuwasisitiza kutosimamisha magari sehemu zisizo rasmi kwaajili ya abiria kujisaidia, amesema suala hilo maarufu kama kuchimba dawa ni kosa kisheria na sio salama kwa wananchi kujisaidia vichakani na wanaweza pia kuwasababishia ajali kutokana na madereva kusimamisha magari maeneo ambayo sio salama, badala yake amewataka kusimamisha magari maeneo ambayo yamejengwa vyoo na yameandaliwa rasmi kwa abiria kupata huduma hiyo.PICHA NA JESHI LA POLISI.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...