Mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amechaguliwa tena katika nafasi hiyo baada ya kupata kura 886 sawa na 93.5% dhidi ya mpinzani wake Cecil Mwambe aliyepata kura 59 sawa na 6.2%. 

Wagombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Chama Taifa (Bara) walikuwa wagombea wawili,Tundu Lissu na Sophia Mwakagenda, Lissu amepata kura 930 sawa na 98.8% huku Mwakagenda (aliyetangaza kujitoa akiwa ukumbini) akipata kura 11 sawa na 1.2%.

Nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa Zanzibar ambayo ilikuwa na mgombea mmoja, Said Issa Mohamedi, ameshinda kwa kura za ndio 839 sawa na asilimia 88.7,kura za hapana zilikuwa ni 95 sawa na asilimia 10 na zilizoharibika 12 sawa na asilimia 1.3.

Uchaguzi huo umefanyika katika ukumbi wa Mlimani City na kuhudhuliwa na wanachama na wajumbe wa chama hicho kwaajili ya uchaguzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...