KAMPUNI ya Wananchi Group Ltd hapa nchini Tanzania  imetoa kauli kwa vyombo vya habari ya kumtangaza rasmi, Meneja Mkazi nchini Tanzania wa Wananchi Group kupitia Kampuni hiyo,Sanctus Mtsimbe.

Taarifa ya Kampuni hiyo kwa vyombo vya habari ambayo wametoa leo jijini Dar es Salaam kuwa kampuni yao amemteua  Kennedy Ojungo kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya simbaNet. 

Imeeleza kwamba Ikampuni hiyo inatoahuduma tofauti tofauti  katika nchi nyingi barani Afrika ambapo miongoni mwa nchi zilizokuwa zinafanya kazi na kampuni hiyo ni pamoja Kenya, Uganda, Tanzania, Malawi na Zambia. 

Aidha katika taarifa hiyo ilisema Mtsimbe amepitia katika uongozi mbalimbali ikiwemo Ofisa Mwandamizi wa SimbaNet Afrika  Mashariki, pia tayari aliwahi kuwa na nafasi ya Meneja Mkuu wa Teknolojia ya Mawasiliano ya Airsys (Uingereza) na Meneja Mauzo wa Mkoa kwa Mawasiliano ya Danimex ya nchini  Denmark. 

Pia Kennedy ana uzoefu mkubwa katika tasnia ya Mawasiliano baada ya kufanya kazi katika uwezo wa juu wa mashirika anuwai ya kimataifa.  Aidha Kikundi cha Wananchi hufanya biashara mbalimbali ikiwemo mawasiliano ya makazi, mtandao na huduma za burudani na huduma za mawasiliano ya biashara .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...