Mwanariadha Eliud Kipchoge amejishindia taji la BBC la kuwa ''Mwanamichezo Bora wa mwaka Duniani''.

Kipchoge alikuwa mtu wa kwanza katika historia ya mbio za Marathon kukimbia kilomita 42 kwa muda wa chini ya saa mbili Oktoba, 2019.

Raia huyo wa Kenya, 35, alikamilisha muda wa kilomita 42.2 katika saa moja dakika 59 na sekunde 40 katika shindano la Ineos Challenge mjini Vienna nchini Austria.

Miezi sita kaba ya ushindi wake, Kipchoge alikuwa ameshinda ubingwa wa London Marathon mara nne mfululizo.

Kipchoge, alipata medali ya dhahabu katika mbio za Marathon, Rio 2016, na kuvunja rekodi yake mwenyewe ya London aliyoiweka 2016, kwa sekunde 28.

Kupitia kura zilizopigwa kwa njia ya mtandao, Kipchoge amewashinda mwanariadha wa mazoezi ya viungo Simone Biles, nahodha wa timu ya taifa ya Raga ya Afrika Kusini Siya Kolisi, mchezaji Kriketi wa Australia Steve Smith, mchezaji gofu duniani Tiger Woods na mshambuliaji wa Marekani Megan Rapinoe, ambaye aliongoza tena timu yake katika mashindano ya Kombe la Dunia msimu wa joto uliopita.

Mshindi wa mwaka jana alikuwa mchezaji gofu Francesco Molinari, aliyeshinda mashindano ya Dunia 2018, pamoja na mashindano yote matano ya mechi za kombe la Ryder mjini Paris.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...