Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Riziki Pembe Juma akitoa
nasaha kwa wahitimu wa kada mbali mbali katika Chuo Kikuu cha Taifa
Zanzibar University ( ZU) wakati wa mahafali 17 ya chuo hicho huko
Tunguu Wilaya ya Kati Unguja .
Baadhi ya wahitimu wa chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar University
wakitunukia vyeti wakati wa Mahafali 17 ya chuo hicho huko Tunguu
Wilaya ya Kati Unguja .
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Riziki Pembe Juma
akimkabidhi Cheti cha Elimu ya Master Muhitimu Khamisuu Hamid Mohamed
huko katika Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar University Tunguu Wilaya ya
Kati Unguja .
Baadhi ya Wahitimu wa kada mbali mbali wakimsikiliza Waziri wa Elimu na
Mafunzo ya Amali Riziki Pembe Juma ( hayupo pichani) akitoa nasaha kwa
wahitimu wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar University ( ZU)wakati wa
Mahafali 17 ya chuo hicho huko Tunguu Wilaya ya Kati Unguja .
Na Rahma Khamis Maelezo Zanzibar
Wahitimu wa vyuo vikuuu wametakiwa kulipa mikopo waliopatiwa na Bodi ya Mikopo Zanzibar kwa ajili ya masomo yao ili na wengine wapate fursa hiyo ya kuendeleza masomo yao.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Riziki Pembe Juma wakati wa mahafali ya 17 ya kuwatunukia vyeti wahitimu wa fani mbali mbali katika Chuo kikuu cha taifa Zanzibar University ( ZU) Tunguu Wilaya ya Kati Unguja
Amesema iwapo wahitimu hawatoweza kulipa mikopo waliopatiwa kwa wakati muwafaka, watasababisha wengine kupata fursa ya mikopo hiyo jambo ambalo ni kinyume na utaratibu wa bodi hiyo.
Amesema kuwepo kwa University Zanzibar kumeleta maendeleo ya kiuchumi visiwa vya Zanzibar,Tanzania na Afrika kwa ujumla na kumesaidia ongezeko kubwa la wanafunzi katika mwaka huu kulinganisha na mwaka uliopita ambao ulitoa wahitimu 9344 katika kada tofauti 4516 wanaume na 4828 wanawake ambao wapo Serikalini na sekta binafsi.
Aidha Waziri Pembe amefahamisha kuwa kabla ya Mapinduzi ya Zanzibar kulikua kuna idadi ndogo ya wahitimu wa Vyuo Vikuu, ukilinganisha na hali ilioyopo hivi sasa na wahitimu wanaume waliongoza katika kufaulu kuliko wanawake. kutokana na mfumo dume uliokuwepo awali,baada ya kuwepo sayansi na teknololojia wanawake wengi wanajipatia elimu kwa idadi kubwa ya ufaulu wa hali ya juu .
Nae katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Idriss Muslih Hijja amesema Zanzibar University ni chuo cha mwanzo kinachoongeza kada za masomo mbali mbali na wanatarajia kuongeza miundombinu ya vifaa vya masoma ili kuleta maendeleo kwa wanafunzi waliopo hapo.
Hata hivyo amesema kuwa mpango uliopo kwa sasa ni kujenga jengo jipya na kutoa ofisi mbali mbali ili kutatua tatizo hilo na kutafuta miradi mbalimbali ya kuongeza kipato kwa wanafunzi na walimu jambo ambalo litasaidia ufanyaji kazi kwa ufanisi mkubwa
Kwa upande wa wahitimu wa Chuo hicho akiwemo Pili Sheha Khamisi kwa niaba ya wenzake wameiomba Serekali kuwapatia ajira ili waweze kulipa mkopo waliopatiwa.
Wahitimu wa vyuo vikuuu wametakiwa kulipa mikopo waliopatiwa na Bodi ya Mikopo Zanzibar kwa ajili ya masomo yao ili na wengine wapate fursa hiyo ya kuendeleza masomo yao.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Riziki Pembe Juma wakati wa mahafali ya 17 ya kuwatunukia vyeti wahitimu wa fani mbali mbali katika Chuo kikuu cha taifa Zanzibar University ( ZU) Tunguu Wilaya ya Kati Unguja
Amesema iwapo wahitimu hawatoweza kulipa mikopo waliopatiwa kwa wakati muwafaka, watasababisha wengine kupata fursa ya mikopo hiyo jambo ambalo ni kinyume na utaratibu wa bodi hiyo.
Amesema kuwepo kwa University Zanzibar kumeleta maendeleo ya kiuchumi visiwa vya Zanzibar,Tanzania na Afrika kwa ujumla na kumesaidia ongezeko kubwa la wanafunzi katika mwaka huu kulinganisha na mwaka uliopita ambao ulitoa wahitimu 9344 katika kada tofauti 4516 wanaume na 4828 wanawake ambao wapo Serikalini na sekta binafsi.
Aidha Waziri Pembe amefahamisha kuwa kabla ya Mapinduzi ya Zanzibar kulikua kuna idadi ndogo ya wahitimu wa Vyuo Vikuu, ukilinganisha na hali ilioyopo hivi sasa na wahitimu wanaume waliongoza katika kufaulu kuliko wanawake. kutokana na mfumo dume uliokuwepo awali,baada ya kuwepo sayansi na teknololojia wanawake wengi wanajipatia elimu kwa idadi kubwa ya ufaulu wa hali ya juu .
Nae katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Idriss Muslih Hijja amesema Zanzibar University ni chuo cha mwanzo kinachoongeza kada za masomo mbali mbali na wanatarajia kuongeza miundombinu ya vifaa vya masoma ili kuleta maendeleo kwa wanafunzi waliopo hapo.
Hata hivyo amesema kuwa mpango uliopo kwa sasa ni kujenga jengo jipya na kutoa ofisi mbali mbali ili kutatua tatizo hilo na kutafuta miradi mbalimbali ya kuongeza kipato kwa wanafunzi na walimu jambo ambalo litasaidia ufanyaji kazi kwa ufanisi mkubwa
Kwa upande wa wahitimu wa Chuo hicho akiwemo Pili Sheha Khamisi kwa niaba ya wenzake wameiomba Serekali kuwapatia ajira ili waweze kulipa mkopo waliopatiwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...