Mstahiki Meya wa Halmashauri ya
Manispaa ya Kinondoni, Mhe. Benjamini Sita akipokea mashuka na foronya
zilizotolewa na vikundi vya ushirika vya Halmashauri hiyo, wanaoshuhudia
ni wanakikundi hao pamoja na Mkuu wa Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na
Ushirika wa Halmashauri hiyo Ndugu Salehe Hija .
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya
Manispaa ya Kinondoni, Mhe. Benjamini Sita akikata utepe kwa ajili ya
kuzindua mfumo wa usomaji data leo wakati alikuwa akikabidhiwa vifaa vya
Hospital na vyama vya ushirika kutoka katika Halmashauri hiyo.
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya
Manispaa ya Kinondoni Mhe. Benjamini Sita , akizungumza na vikundi vya
ushirika wakati akikabidhiwa vifaa vya Hospital vilivyotolewa na vikundi
hivyo. Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na
Ushirika wa Halmashauri hiyo Ndugu Salehe Hija .
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya
Manispaa ya Kinondoni, Mhe. Benjamini Sita akisamiliana na Mkuu wa
Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika wa Halmashauri hiyo Salehe
Hija.
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya
Manispaa ya Kinondoni, Mhe. Benjamini Sita akimkabidhi mashuka Mganga
mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Kigogo mara baada ya vyama hivyo
kumkabidhi vifaa hivyo.
Mkuu wa Idara ya Kilimo,
Umwagiliaji na Ushirika wa Halmashauri hiyo Ndugu Salehe Hija, mwenye
miwani akimueleza jambo Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya
Kinondoni, Mhe. Benjamini Sita wakati alipokuwa akipokea magodoro
kutoka vikundi vya ushirika.
***************************
Mstahiki Meya wa
Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Mhe. Benjamini Sita amevipongeza
vyama vya ushirika vilivyopo katika Halmashauri hiyo kwa kujitolea vifaa
vya Hospitali katika Kituo Cha Afya cha Kigogo.
Aidha vyama hivyo
vimemkabidhi Mhe. Sita Magodoro 30, mashuka na foronya 150 ambapo
wamesema kuwa vitasaidia wagonjwa watakaokuwa wanapatiwa matibabu katika
kituo hicho.
Akizungumza na
vyama hivyo kabla ya kukabidhiwa vifaa hivyo, Meya Sita amesema kuwa
vitasaidia kuwahudumia wananchi mbalimbali watakao kuwa wanapatiwa
huduma katika Kituo hicho cha Afya na kuwasihi wengine kujitokeze
kuchangia.
Amefafanua kuwa
suala la Afya ni pana na kwamba Halmashauri iliamua kujenga Kituo hicho
cha Afya ili kuwezesha wananchi kupata huduma kwa haraka na urahisi
kutoka maeneo mbalimbali.
Ameeleza kuwa,
Halmashauri ya Kinondoni inahudumia watu kutoka sehemu mbalimbali
ikiwemo Bagamoyo, na kwamba kulingana na wingi huo, imeweza kununua
eneo hilo na kujenga Kituo hicho cha Afya na kwamba watu kutoka shemu
mbalimbali watapata huduma safi na bora inayokidhi viwango.
Ameongeza kuwa”
Tumepambana usiku na mchana, na mpongeza sana Mkurugenzi wetu , Ndugu
Aron Kagurumjuli na watendaji wote kwa kufanikisha ujenzi wa Kituo hichi
cha Afya, ambacho kitahudumia watu sio Kigogo tu , bali kitatoa huduma
Ilala, Ubungo, na maeneo mengine kama ilivyo kwa Kituo cha Afya cha
Magomeni.” amesema Meya Sita.
Hata hivyo Mhe.
Sita emesema “ ninawapongeza sana, ninaimani wadau wengine watakapo ona
hivi, itawakumbusha kuona kwamba wanawajibu kufanya hivi kama
walivyofanya hawa vyama vya ushirika kutambua umuhimu wa afya katika
Halmashauri yetu” ameongeza.
Kwa upande wake
Mkuu wa Idara ya Kilimo, Umwagiliaji, na Ushirika , Ndugu. Salehe Hija
amekipongeza kitengo cha ushirika kwa kuandaa vifaa hivyo na kukabidhi
katika Kituo hicho cha Afya na kusema kuwa kitendo hicho kitaonyesha
njia kwa watu wengine kujitolea.
Aidha Hija
amesema kuwa vifaa hivyo vilivyotolewa vinathamani ya shilingi milioni
6.7 huku kituo hicho kikiwa na uhitaji wa vitanda 150 ambapo kwa
mujibu wa mganga mfawidhi wa Kituo hicho , magodoro hayo yaliyotolewa
ni ni sawa na asilimia 20 ya mahitaji hayo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...